• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YA SONGEA YAKUSUDIA KUJENGA SOKO LA KISASA MANZESE 'A' IFIKAPO JULAI 2022.

Tarehe ya kuwekwa: December 8th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

08.12.2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea yajipanga kuanza ujenzi wa soko la kisasa  Manzese A ifikapo Julai 2022.

Hayo yamebainishwa na Mratibu Msaidizi wa Kitengo cha Uratibu wa Miradi ya Benki ya Dunia cha Ofisi ya Rais - TAMISEMI (WBCU) Rashid Mtamila wakati akitoa mafunzo kuhusiana na utekelezaji wa mradi wa kuboresha miundombinu na utendaji kazi ndani ya Halmashauri za miji (TACTIC),  kwa wataalamu na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea leo tarehe 08 Disemba 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea.

Mtamila alieleza kuwa lengo la mradi huo ni kuziboresha Halmashauri ili ziweze kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuboresha miundombinu ndani ya Halmashauri za miji nchini Tanzania ambapo kiasi cha shilingi Trilioni moja na bilioni 150 kimetolewa kutoka benki kuu ya dunia ambazo zitagawanywa katika Halmashauri za miji 45 nchini.

Aliongeza kuwa mgawanyo wa fedha hizo utakuwa katika awamu tatu ambapo awamu ya kwanza fedha hizo zitatolewa kwa Halmashauri za miji 12 ikiwemo na Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kuboresha miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami, madaraja, maeneo ya kutupa taka pamoja na ukarabati wa masoko ikiwemo na soko la Manzese.

Akibanisha Halmashauri za miji zitakazonufaika mradi huo kwa awamu ya kwanza ni pamoja na Ilemela MC, Mwanza CC, Geita TC, Kahama MC, Tabora MC, Kigoma ujiji MC, Arusha CC, Dodoma CC,Morogoro MC, Sumbawanga MC, Mbeya CC, na Songea MC.

Alisema kuwa  mradi wa TACTIC umelenga kupunguza changamoto ya upungufu wa miundombinu bora katika miji hali inayotokana na ongezeko la watu katika maeneo ya mjini na hivyo kusababisha miundombinu iliyopo kushindwa kukidhi mahitaji ya idadi ya watu inayoongezeka kila mwaka.’Mtamila Alibainisha’

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Sustainability Associate Ltd  Kayonko Juma Kayonko amewataka wataalamu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuhakikisha wanawashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo na wafanyabiashara pamoja na wakazi wa maeneo hayo kwa lengo la  kupata maoni yao kabla ya utekelezaji wa mradi kuanza ili kuondoa migogoro na malalamiko yanayoweza kujitokeza.

Aidha, Mkuu wa kituo kikuu cha polisi Songea SP. Saana Mdatu amewataka wataalamu kuhakikisha wanazungumza na wadau waliopo katika maeneo ambayo miradi hiyo itatekelezwa ili kuweka makubaliano ambayo hayatasababisha uvunjifu wa Amani katika kipindi cha utekelezwaji wa mradi huo.’Alisisitiza’

Akitoa shukrani kwa niaba ya viongozi na wananchi wa kata ya Misufini, Diwani wa kata hiyo Mh. Ismail Azizi ameishukuru Serikali kwa kutoa fedha hizo kwa ajili ya kuboresha soko la Manzese pamoja na kutengeneza lami kilomita 3 kuzunguka soko hilo ambalo lipo katika eneo la kata yake na kusaidia kuinua uchumi kwa kutoa ajira kwa wananchi waliopo katika eneo hilo.

Naye Katibu wa wamachinga Manispaa ya Songea Mohammed Sulemani alisema kuwa mradi huu utaleta tija kwa wananchi hususani kwa wajasiriamali ambao wataweza kufanya biashara kwenye maeneo mazuri yalioboreshwa.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa