• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA UKAMILISHAJI WA UJENZI WA MADARASA YA UVIKO 19

Tarehe ya kuwekwa: December 16th, 2021

Na;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA 

16 DISEMBA 2021

Mkurugenzi Msaidizi  Idara ya Serikali za Mitaa sehemu ya utoaji huduma na Utawala Bora (TAMISEMI)  Angelista Kihaga amewataka viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kuweka utaratibu wa kufanya vikao  mara kwa mara kwa kushirikisha kamati za shule,  waheshimiwa Madiwani, Walimu na uongozi wa Serikali za mitaa ili kupokea changamoto zinazoikabili shule hususani miundombinu ya shule.

Hayo yamebainishwa  leo   tarehe 16 disemba 2021   katika  ziara ya siku moja  iliyofanyika Manispaa ya Songea yenye lengo la kukagua ujenzi wa madarasa uliokuwa ukisimamiwa na  kamati ya ujenzi wa miradi hiyo ili kutekeleza Mpango wa maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19,   ambapo alifanikiwa kutembelea  Shule ya Sekondari Matogoro, shule ya Sekondari Msamala, shule ya Sekondari Londoni, shule ya sekondari Lizaboni na Shule ya sekondari  Mfaranyaki.

Kihaga amewapongeza viongozi na Wataalamu wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa jitihada za usimamizi bora wa ujenzi wa madarasa 29 yenye thamani ya Shilingi 660,000,000 ambao ulianza tarehe 01 novemba 2021 na kukabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya tarehe 11 disemba 2021 ukiwa tayari  umekamilika kwa asilimia 100%.  “Kihaga aliwapongeza”

Amewarai Wananchi wote  kuendelea kujitolea pamoja na kuchangia nguvu kazi kupitia mitaa yao ili kusaidia kupunguza kero za miundombinu mbalimbali za shule pamoja na kuimarisha hali ya ufaulu wa wanafunzi katika halmashauri.

Amewataka wataalamu wa ujenzi kuendelea kusimamia miradi ya ujenzi yote inayoendelea kujengwa bila kujali upungufu wa wataalamu hao wa ujenzi kwani kwa kufanya hivyo  kutakuwa na mafanikio chanya ya utekelezaji kwa kila mradi utakaopangwa  kujengwa.

Waheshimiwa madiwani kwa nyakati tofauti nao wametoa shukrani kwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha katika Halmshauri na kufanikiwa kujenga madarasa 26 ya Sekondari na madarasa 3 shule za msingi ili   kupunguza changamoto za madarasa na samani za shule.

Wanafunzi wa Sekondari na Msingi  nao wameipongeza Serikali  kwa kuwezesha kujenga miundombinu ya madarasa  ambapo walizitaja faida za kuwepo kwa miundombinu rafiki ya kujisomea ikiwemo  na uwepo wa ufaulu mzuri, kupata usikivu darasani, pamoja na kuondoa kero ya mlundikano  wa wanafunzi wawapo madarasani.

Mwisho

  

   

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa