• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA ya Songea yatoa mbegu bora za ufuta bure kwa Wakulima 100.

Tarehe ya kuwekwa: November 24th, 2020

 Halmashauri ya Manispaa ya Songea imewainua wakulima wa zao la biashara la Ufuta kwa kuwapatia mbegu bora za ufuta kwa wanavikundi 3 vitatu pamoja na AMCOS ili kuepukana na kutegemea zao moja la mahindi ambalo ni zao kuu la chakula.

Hayo yamebainishwa na Afisa kilimo wa Manispaa ya Songea Zawadi Nguaro  katika mafunzo kwa wanavikundi  vya wakulima wa ufuta kutoka kata ya Lilambo,Mletele, Subira, pamoja na kikundi cha wakulima wa AMCOS Songea yanayoendeshwa  na Halmashauri ya Manispaa ya Songea,  ambayo yanayoendelea kufanyika  kwa muda wa siku tatu kuanzia 23 – 25/11/2020.

 Nguaro “ alisema Halmashauri ya manispaa ya Songea ina kata 21, kati ya kata hizo ni kata tatu ambazo zimeanza  kupata mafunzo kwa wanavikundi wa  kilimo bora cha ufuta  kwa lengo la kutoa elimu kwa wakulima  ili waweze kulima zao bora la biashara la ufuta  kwa ajili ya kuinua kipato cha mkulima na kuondoa dhana ya  kulima zao moja la mahindi pekee.

 Alisema kazi ya Halmashauri ni kutoa Elimu endelevu kwa wakulima pamoja na kuwawezesha mbegu bora ya ufuta  kilo mbili 2 kwa kila mwanakikundi aliyeshiriki mafunzo hayo, kwa  idadi ya wanachama  25 kwa kila kikundi.

 Amewataka washiriki wa mafunzo hayo  kuwa wasikivu na kufuata maelekezo yote yatakoyotolewa na wawezeshaji wa mafunzo hayo ili waweze kujiinua kipato kwa kuuza mazao yao kwa kutumia mfumo wa stakabadhi gharani  kwa kupeleka mavuno yao kwenye chama cha Msingi cha WEST AMCOS kilichopo Manispaa ya Songea ili kuondoa unyonyaji kwa wakulima.

 Naye Afisa kilimo kata ya Matogoro Salumu   Mkwamba alibainisha kuwa zao la ufuta ni zao la biashara ambalo mbegu zake zina kiasi kikubwa cha mafuta kiasi cha asilimia 45% hadi asilimia 55% ambapo mafuta ya ufuta yanathamani kubwa hivyo hulifanya kuwa zao bora la biashara.

Zao la ufuta hustawi katika maeneo yenye udongo mwepesi mweusi na usio tuamisha maji na udongo tifu tifu ambapo aliongeza kuwa mbegu za asili zina uwezo wa kutoa mavuno kidogo na huchukua siku 140 hadi 180 kukomaa na hutoa mavuno kati ya kilo 150 hadi 300, na ikiwa utatumia mbegu za kisasa  zinauwezo wa kukomaa kwa muda mfupi na hutoa mavuno mengi kwa wastani wa  kilo 500-1000 lakini hutegemeana na huduma. “ Alibainisha Mkwamba”

Akiitaja aina za mbegu za kisasa ni pamoja na naliendele 92, Lindi 202, Ziada 94, Mtwara, Lindi White, na Naliendele 2002. Zao la ufuta kwa Tanzania hulimwa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Manyara, Pwani, Singida  na Tanga. Nk.

  

IMETAYARISHWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

24.11.2020

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa