• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA YA SONGEA YAVUNJA MKATABA NA LUKOLO

Tarehe ya kuwekwa: October 10th, 2017

MANISPAA YA SONGEA YAVUNJA MKATABA NA LUKOLO

HATIMAYE Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma imevunja rasmi Mkataba wa ujenzi wa lami nzito kati yake na Kampuni ya Lukolo yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Eng.Samwel Sanya amesema muda wa Mkataba wa kumaliza kazi kwa Mkandarasi huyo ulimalizika tangu Juni 30 mwaka huu.

Amesema baada ya muda huo kumalizika Mkandarasi huyo aliingizwa kwenye tozo(Liquidated Damage) na kwamba iwapo atashindwa kumaliza kazi kwa siku 100 hatua za kisheria za kuvunja mkataba zitafanyika.

“Oktoba 8,2017 ndiyo siku 100 alizopewa Mkandarasi huyo zimemalizika hivyo tumevunja mkataba rasmi na Mkandarasi huyo,amekatwa asilimia 10 ambayo ni sawa na sh.bilioni 1.4 kwa kuchelewesha mradi na anatakiwa kulipa asilimia 15 ya fedha kwa kazi ambazo hajamaliza ndani ya mkataba’’,anasisitiza  Sanya.

Mkandarasi huyo pia anatakiwa kurudisha kiasi cha shilingi bilioni 2.15 kiasi cha fedha ambacho kilitolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB),fedha ambazo zilitolewa kwa ajili ya kusafirishia mitambo mbalimbali ya ujenzi katika mradi huo.

Kaimu Mkurugenzi huyo wa  Manispaa ya Songea amesema  baada ya kuvunjwa mkataba huo,Manispaa inaanza mchakato wa kumtafuta Mkandarasi mwingine ili kuendeleza kazi ya ujenzi wa barabara na kwamba Manispaa haijapata hasara yeyote baada ya kuvunjwa kwa mkataba huo.

Zaidi ya sh.bilioni 14 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa barabara za Mji wa Songea katika kiwango cha lami nzito zenye urefu wa kilometa 8.6.

Fedha za mradi huo zimetolewa na Benki ya Dunia chini ya Mpango wa kuzijengea uwezo serikali za mitaa(ULGSP), mpango huo unakusudia kuendeleza miundombinu ya Halmashauri za miji na Manispaa 18 za Tanzania Bara ikiwemo Manispaa ya Songea.

Mradi huo ambao ulianza Juni Mosi 2015 ulitarajiwa kukamilika Juni 30,2017 ambapo fedha iliyopokelewa na Manispaa ni  zaidi ya sh.bilioni saba ambapo hadi sasa Mkandarasi ameshalipwa zaidi ya sh.bilioni nne.

Barabara za Manispaa ya Songea ambazo zipo kwenye mradi huu ni FFU hadi Matogoro yenye urefu wa kilometa 3.2,barabara ya Songea Girl’s hadi Mateka yenye urefu wa kilometa 1.5 na barabara ya Mwembechai hadi Bombambili yenye urefu wa kilometa 2.6.

Barabara nyingine ni Mitumbani hadi Yapenda yenye urefu wa kilometa moja,barabara ya Polisi hadi Stendi ya Mlilayoyo yenye urefu wa kilometa 0.45.

Taarifa imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea              

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa