HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/2018 imeidhinishiwa zaidi bilioni 15 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Tina Sekambo amesema kati a fedha hizo zaidi ya shilingi bilioni sita ni za ndani na zaidi ya bilioni tisa ni fedha za nje.
Sekambo anabainisha kuwa fedha ambazo zimepokelewa toka hazina katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Septemba 2017 ni zaidi ya bilioni tatu na kwamba kati ya fedha hizo zaidi ya bilioni 3.5 ni fedha za mradi wa uboreshaji na uendelezaji wa miji(ULGSP).
Hata hivyo amesema fedha hizo ni bakaa ya mwaka wa fedha wa 2016/2017 ambapo zaidi ya shilingi milioni 340 ni fedha zinazopokelewa toka hazina pamoja na mapato ya ndani katika kipindi cha mwaka 2017/2018 sawa na asilimia 9.7 ya fedha zilizotakiwa kupokelewa katika robo ya kwanza katika bajeti ya mwaka 2017/2018.
Imetolewa na Albano Midelo
Afisa Habari Manispaa ya Songea
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa