• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MANISPAA yakabidhi mradi wa maji RUHUWASO

Tarehe ya kuwekwa: May 7th, 2018

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea imekabidhi rasmi mradi wa maji kwa Jumuiya ya Watumia Maji wa Ruhuwiko Kanisani(RUHUWASO),ambao ulifadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 429.65

Makabidhiano ya mradi huo yamefanyika Mei 5,2018 katika ofisi za Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani na kuhudhuriwa na wananchi wa Mtaa huo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Diwani wa Kata na viongozi wa RUHUWASO.

Akizungumza kabla ya kukabidhi mradi huo,Mhandisi wa Maji Manispaa ya Songea Mhandisi Samwel Sanya amesema  mradi huo umekabidhiwa kwa RUHUWASO ili waweze kuutunza,kuulinda na kuuendesha bila kuitegemea Halmashauri na kwamba Halmashauri itaendelea kutoa huduma za ushauri na kitalaam.

Hata hivyo mara baada ya Manispaa kukabidhi mradi huo kwa RUHUWASO nao  waliukabidhi kwa Mamlaka ya Maji Safi Songea(SOUWASA) ambao kulingana na sheria SOUWASA wana mamlaka ya kuingiza maji ndani ya nyumba.

“Kwa sababu Mtaa wa Ruhuwiko kanisani upo ndani ya mji na sio pembezoni na wananchi wengi wanahitaji kuingiziwa maji ndani hivyo wananchi wameamua jambo la busara kukabidhiwa mradi kwa SOUWASA’’,anasisitiza Mhandisi Sanya.

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imekabidhi mradi huo kwa RUHUWASO ukiwa na vyanzo viwili vya maji vilivyo chini ya ardhi,nyumba mbili za mitambo,birika la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 135,000,mtandao wa maji wenye urefu wa kilometa tisa,vituo 16 vya kuchotea maji,birika tatu za uvunaji wa maji ya mvua na vyumba 25 vya vigawo vya maji.

Mradi wa maji katika Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani, uliibuliwa na Wananchi wenyewe mwaka wa fedha 2013/2014 na kuanza kujengwa mwaka wa fedha 2014/2015,Mkandarasi akiwa ni Girafe Investment Company.

Watu wapatao 3,447 kutoka katika Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani wanatarajia kunufaika na mradi huo wa maji safi na salama baada ya mradi kukamilika,

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Mei 6,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa