• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MBUNGE WA JIMBO LA SONGEA MJINI AZINDUA MIRADI YA UVIKO-19 KATA YA SUBIRA.

Tarehe ya kuwekwa: November 1st, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

01.11.2021

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imezindua rasmi miradi ya kuboresha miundombinu ya afya na elimu kwa lengo la kuanza utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu hiyo.

Miradi hiyo ilizinduliwa na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro iliyofanyika katika kata ya Subira Manispaa ya Songea 31 Oktoba 2021 ambayo ilihusisha ujenzi wa madarasa mawili pamoja na mradi wa maji utakaojengwa katika Kata hiyo pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi katika Bwalo la chakula katika Sekondari ya Emanuel Nchimbi.

Dkt. Ndumbaro alisema kuwa fedha hizo zilizotolewa haziwezi kutatua changamoto zote zilizopo na hivyo amewataka wananchi kuchangia nguvu zao ili kuokoa kiasi cha fedha  ili ziweze kuongeza mradi mwingine. Ikumbumbukwe ya kuwa Manispaa ya Songea imepokea fedha million 660,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika Sekondari 26, ujenzi madarasa katika vituo shikizi kwa shule za msingi Nonganonga pamoja na ujenzi wa bwalo la chakula kwa shule yenye wanafunzi wenye mahitaji maalmu katika shule ya Msingi Ruhila.

Aliongeza kuwa Manispaa ya Songea imejipanga kujenga mradi wa gofu ambao utasaidia kujenga hoteli kubwa 5 na kuongeza fursa za ajira kwa vijana pamoja na kuleta maendeleo na kuboreshwa kwa miundombinu ya barabara kama ilivyo kwa mji mitano pekee nchini Tanzania yenye viwanja vya gofu ambayo ni Dar es Salaam, Moshi, Arusha, Morogoro na Mufindi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Songea kusimamia wahandisi wote kwa kuhakikisha wanakuwepo kwenye maeneo ya ujenzi wa miradi  ili waweze kusimamia kwa ufanisi na kwa  uhakika wa ubora wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Kamando amesisitiza kuwa miradi hiyo inatakiwa kutekelezwa kwa wakati ambapo hadi kufikia tarehe 15 Disemba 2021 miradi hiyo itakabidhiwa rasmi kwenye tathimini ya Mkoa wa Ruvuma na hivyo wataalamu wahakikishe   wanakuwa makini katika kusimamia  zoezi hilo.

Amewataka viongozi wa Serikali za mitaa kufanya mikutano ya hadhara kwenye maeneo yao ili kuendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika utekelezaji wa miradi hiyo kwa kuhakikisha maeneo yaliyochaguliwa kujenga miradi hiyo hayabadilishwi.

Nae Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Hamisi Abdallah Ally amewataka wananchi kutoa ushirikiano wakati wa ujenzi wa madarasa hayo ili kufanikisha ujenzi huo.

Akitoa ufafanuzi kuhusiana na kupanda kwa bei ya mbolea alisema kuwa tatizo la kupanda kwa bei ya mbolea imetokana na kufungwa kwa viwanda  vya kuzalisha mbolea kutoka nchi za nje zilizoendelea kutokana na ugonjwa wa UVIKO 19.” alibainisha”

Ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa hatari wa UVIKO 19 pamoja na kuendelea kupata chanjo kwa hiari ya ugonjwa huo.

Mwisho.

.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa