Na; Amina Pilly
Songea, 14 Juni 2025 – Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Mhe. Michael Mbano, ametoa wito kwa familia zote kushiriki kikamilifu katika uchangiaji wadamu kwa hiari, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu kuhakikisha upatikanajiwa damu salama wakati wa dharura na kuokoa maisha ya wanajamii.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Mchangia Damu Kitaifa, yaliyofanyika katika viwanja vya Bustani ya Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma ambapo Wikihiyo ilianza tarehe 01 Juni 2025 na kufikia tamati leo, tarehe 14 Juni 2025,siku ambayo dunia huadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani.
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma alisema, Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022,Mkoa wa Ruvuma una takribani watu milioni 1.8, ambapo unahitaji chupa 14,789 za damu kila mwaka. Hata hivyo, kwa mwaka 2024, mkoa uliweza kukusanya chupa 7,016 tu, sawa na 47%ya mahitaji ya kila mwaka. Katika kipindi cha Januari hadi 12 Juni 2025, jumlaya chupa 4,040 zilikusanywa,sawa na 27% ya lengo la mwakahuu.
Aidha, alifafanua kuwa watumiaji wakubwa wadamu salama ni:Watoto chini ya miaka 5 (50%), Mamawajawazito (30%), Wahanga wa ajali, wagonjwa wa ndani, nawanaohitaji upasuaji (20%)
Kwa upande wake, Mganga Mkuu Msaidiziwa Mkoa wa Ruvuma, Dkt. Chihoma Mhako, alieleza kuwa damu haiwezi kutengenezwa kiwandani au kuuzwa madukani, hivyo ni muhimu jamii ichangie kwahiari.
Alibainisha kuwa katika wiki ya mchangia damu pekee, zilikusanywa chupa 1,213, sawa na 17.16% ya lengo la wiki ya kuchangia damu(chupa 1,035).
Mhe. Mbano alihitimisha kwa kusisitiza kuwa "ni wajibu wa kila familiana mwanajamii kuhakikisha anachangia damu mara kwa mara, kwa kuwa damu huokoamaisha – si kwa wageni tu, bali kwa familia zetu wenyewe."
SONGEA MUNICIPAL COUNCIL
Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA
Simu ya Mezani: 025 2602970
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@songeamc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa