• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MFAHAMU aliyegundua kuteketea kwa makaa ya mawe ya Ngaka

Tarehe ya kuwekwa: April 8th, 2018

HIVI karibuni Rais wetu Dkt.John Magufuli amemzawadia kiasi cha shilingi milioni 100 Mzee Jumanne Ngoma aliyegundua madini ya Tanzanite mwaka 1967 katika eneo la Mirerani mkoani Manyara.

Tunampongeza sana Rais wetu kwa kuwatambua watanzania ambao wameonesha uzalendo katika nchi yao kwa kuvumbua,kugundua na kuzilinda rasilimali za nchi ambazo zinatakiwa kuwanufaisha watanzania wote.

Mzee Benedict Mapunda (Rasha) mwenye umri wa miaka 66 mkazi wa kijiji cha Ntunduwaro ndiye aliyegundua kuteketea kwa moto kwa  mgodi wa madini ya makaa ya mawe Ngaka uliopo Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma mwaka 2006.

Inakadiriwa moto huo uliwaka kwa miaka mitatu kuanzia mwaka 2003 hadi mwaka 2006 uliteketeza tani milioni sita za makaa ya mawe.Inaaminika Moto huo ulianza kuwaka tangu Septemba mwaka 2003.Moto huo usingegundulika mapema ungeweza kuteketeza mamilioni ya tani za makaa ya mawe.

Mzee Rasha anasema katika kipindi chote cha miezi mitatu cha kuzima moto huo alikuwa anasimamia kuhakikisha moto huo unazima kazi ambayo anasema aliifanya kwa uzalendo bila kulipwa kitu chochote na kwamba watalaam baada ya kuchimba na kuweka mchanga,waliondoka na kazi ya uangalizi hadi moto ulipozima mwaka 2006 aliachiwa pekee yake.

Hata hivyo uchunguzi,umebaini Mzee Rasha bado hajatambulika kwa kuokoa rasilimali adimu ya madini ya makaa ya mawe kwa nchi yake ambayo yalikuwa yanateketea kwa moto ardhini kwa miaka kadhaa.Rasha anafanyakazi ambayo haifanani na umri wake katika Kampuni ya TANCOAL kwenye mgodi wa Ngaka.

 Mgodi huo hivi sasa unaingiza mabilioni ya fedha kwa Kampuni  binafsi ya uchimbaji wa madini hayo ya TANCOAL na serikali inalipwa kodi na ushuru kutokana na kazi ya uchimbaji na usafirishaji wa madini hayo ilioanza tangu mwaka 2011.

Kaimu Meneja Mgodi wa Makaa ya mawe Ngaka Edward Mwanga anasema Kampuni ya TANCOAL inatambua mchango wa Rasha kuanzia alipogundua moto wakati unaunguza mgodi,mchango wake katika utafiti na sasa uchimbaji wa makaa ya mawe ndiyo maana hadi sasa licha ya kuwa na miaka 66 bado Kampuni imeamua kuendelea kumwajiri na kumtumia.

Utafiti uliofanywa Mwaka 2001,kwenye mgodi wa Ngaka ulibaini kuwepo kwa madini ya makaa ya mawe yanayoongoza kwa ubora duniani kiasi cha  tani milioni 400 ambazo zinatarajiwa kuchimbwa kwa zaidi ya miaka 50.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manipaa ya Songea

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa