• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MH. WAZIRI WA MAZINGIRA " AKEMEA WANAO CHOMA MOTO MISITU "

Tarehe ya kuwekwa: December 18th, 2021

Na; 

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA 

18 Desemba 2021.

Waziri wa Nchi Ofisi  ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mheshimiwa Selemani Jafo amewataka wananchi na viongozi  kupanda miti million 276 kwa Nchi nzima, kwa  jumla ya   Halmashauri 184  na kila Halmashauri inapaswa kupanda miti Millioni 1.5 kila mwaka.

Hayo yametamkwa na Waziri wa Nchi Ofisi  ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mheshimiwa Selemani Jafo akiwa ziarani Mkoani Ruvuma iliyofanyika leo tarehe 18 mwezi desemba 2021 na kufanikiwa  kutembelea  mradi  wa Machinjio ya kisasa na chanzo cha maji kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kukagua maendeleo halisi ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Jafo alianza kwa kuwapongeza Wataalamu na viongozi wote kwa usimamizi bora wa mradi wa Machinjio mpya ya kisasa yenye uwezo wa kuchinja ng’ombe 300 kwa siku ambapo kwa kwasasa machinjio hiyo imeanza kufanya kazi ya uchinjaji wang’ombe 40 kwa siku.

Akizungumzia suala la utunzaji wa Mazingira alisema“ agenda za  mazingira ni agenda muhimu sana bila kudhibiti uhalibifu wamazingira Nchi yetu itaendelea kuwa katika janga kubwa sana, hivyo amewataka viongozi kuongeza umadhubuti wa kusimamia na kuweka misingi mizuri ili uhalibifu uweze kukomeshwa”. “Mh. Jafo alisisitiza”     

Aliongeza kuwa hivi karibuni katika Nchi yetu imejikuta  imeingia katika changamoto kubwa ya ukosefu wa maji na umeme  hususani katika maeneo ya vijijini, ambapo changamoto ya umeme imeonekana kuwa vyanzo vya maji ambavyo umeme wa maji ulikuwa ukitumia nishati kupitia maeneo mengi sana mabwawa yameendelea kushuka chini  ya kiwango ambapo hupelekea kuwepo kwa mgao mkubwa wa umeme.

Alisema  baadhi ya maeneo mengi ya mekutwa na changamoto ya  maji  hususani maeneo ya vijijini ambapo imetokea  mifugo kukosa malisho bora na maji  ambayo husababisha  baadhi ya wanyama hao kufa. Hivyo amewataka wananchi kuachana na Imani potofu ya kushindana kuchoma misitu ovyo kwa dhana ya kudhani moto ukiuwasha na ukifika mbali utaishi maisha marefu duniani.

Ametoa rai kwa viongozi wote Mkoani Ruvuma kufuata sheria sura namba 20 ya mwaka 2004 ya ambayo inakutaka kuacha kuzingatia mita 60 sitini, pia kwa wale wote watakao bainika wanavunja sheria hiyo wachukuliwe hatua za kisheria.

Naye kaimu Afisa Mazingira Mkoa wa Ruvuma Deogratius Sibula alisema Mkoa wa Ruvuma umekuwa ukiratibu mambo mbalimbali ya usimamizi wa sera na usimamizi wa mazingira ikiwemo na shughuli za usafi wamazingira,  uhifadhi  kwa lengo la kuyafanya mazingira yawe katika hali ya usalama ili kuboresha afya za binadamu na ustawi wa viumbe hai.

Sibula alisema Uzalishaji wa taka Mkoani Ruvuma katika Wilaya zote  ni jumla ya tani 39,596,000 kwa mwaka ambapo sehemu kubwa ya taka ni za majumbani, viwandani na sokoni ambapo asilimia kubwa ya taka hizo hudhibitiwa kupitia mashimo ya taka kwa kuteketezwa kwa moto,  ikiwa  Manispaa ya Songea  huzalisha taka ngumu  tani 71.5  kwa siku

Aliongeza kuwa Halmashauri  zinaendelea kutenga eneo la dampo ikiwemo na Halmshauri ya Manispaa ya Songea inayo eneo lenye mita za mraba 29.3 lililopo kata ya Subira mtaa wa Muungano ambalo limeandaliwa mwaka 2008 na tayari limeshapimwa.

Naye Eng. Francisco Mapunda Mhandisi wa Maji SOWASA alisema Mfumo wa maji safi SOWASA una vyanzo 9 ikiwemo na mlima wa matogoro, Lipasi, Luhira B, Luhira A, Mahilo, zenye  uwezo wa  uzalizashaji   wa Lita Million 11,500,000 wakati wa masika na lita Million 1.438,000 wakati wa kiangazi huku mahitaji halisi Manispaa ya Songea  ni lita Million 17,897,000.

Eng. Mapunda aliongeza kuwa  vyanzo vyote hivyo maji yake hutibiwa na kuchujwa  katika mitambo ya maji safi iliyopo Matogoro yenye uwezo wakutibu  maji lita Milion 11,500,000 kwa siku.

Mwisho.

  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Meya Mbano; Amewataka Wananchi Kulinda Haki za Watoto

    June 16, 2025
  • Meya wa Songea Atoa Wito kwa Familia Kuchangia Damu Kuokoa Maisha.

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

Mbunge Akabidhi Kompyuta 6 na Kufadhili Ukarabati wa Ofisi za Polisi
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa