• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MHE. DIWANI WA KATA YA MJINI AFANYA UHAMASISHAJI WA SENSA MTAA KWA MTAA.

Tarehe ya kuwekwa: August 17th, 2022

Na; 

AMINA PILLY

AFISA HABARI.

17 Agosti 2022 

Mheshimiwa Diwani wa Kata ya Mjini Methew Ngalimanayo amewataka wananchi wa kata ya  Mjini Manispaa ya Songea kutoa ushirikiano kwa makarani wa Sensa pamoja na kushiriki kuhesabiwa  siku ya Sensa itakayofanyika tarehe 23 agosti 2022 ili Serikali iweze kupata takwimu sahihi kwa lengo la maendeleo ya Taifa letu.

Hayo yametamkwa kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa kata ya Mjini uliofanyika  jana tarehe 16 agosti 2022 katika viwanja vya Soko Kuu Songea Mjini ulioshirikisha viongozi  wa dini,  vyama vya siasa Wilaya/kata, wataalamu na vikundi mbalimbali vya ngoma   kwa ajili ya kutoa elimu ya Sensa kwa wananchi wa kata hiyo.

Ngalimanayo alibainisha kuwa  Sensa ilianzishwa mara baada ya nchi mbili kuungana 1964 (Tanganyika na Zanzibar), na baada ya kuungana mataifa yote mawili, mwaka 1967 ilifanyika  Sensa ya kwanza Tanzania kwa lengo la Serikali kupata takwimu za wananchi ili  kupanga maendeleo.


Alisema Serikali huandaa mipango mbalimbali ya maendeleo inayohusu jinsia, watu wenye makundi maalum kama walemavu, watoto, elimu ambapo endapo mwananchi hatatoa taarifa ushirikiano kwa karani wa Sensa serikali haitaweza kupata takwimu sahihi.

Miongoni mwa taarifa zitakazo ulizwa na karani wa Sensa ni pamoja na umri, hali ya ndoa, jinsi, shughuli za kiuchumi, hali ya uzazi, vifo vitokanavyo na uzazi, kilimo, mifugo, uvuvi, misitu, majengo/nyumba na nyinginezo.


Naye mwenyekiti wa CCM Songea Mjini Hamisi Abdallah Ally amewataka wananchi wa kata ya Mjini kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Diwani za kuhamasisha wananchi kushiriki zoezi la Sensa na kukubali kuhesabiwa ili kupata idadi kamili ya Mtaa, kata na Taifa kwa ujumla.


Naye kiongozi wa dini ya kiislamu alisema “Mtume Mohamad (S.W) alihesabiwa Sensa”  alisema Sensa ya Watu na makazi imetamkwa hata katika vitabu vya mungu kwasababu imeeleza kuwa waliteuliwa mitume 25 kwa ajili ya kufanya kazi ya dini katika maeneo mbalimbali kwa maana hiyo ni Sensa. Hivyo amewataka waislamu wote kufahamu kuwa Sensa ipo hata katika maandiko ya mungu.

Naye kiongozi wa dini ya kikristo alisema “Sensa ya mbinguni kuna wenye uhai wanne, wazee wanne wanao kizunguka kiti cha enzi wakitamka neon Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu kwa wakati wa usiku na mchana, wazee 24 katika kiti cha enzi cha yehova ambao wanawakilisha uumbaji wa Mungu, kuna nyota na mwezi ambazo Mungu anafahamu idadi yake.”

Aliongeza kuwa, Yesu alionesha utoshelevu wake kwakulisha wanaume 5000 kwa mikate mitano na samaki mawili wakawalisha wanaume 5000 bila kuhesabu wanawake na watoto, pia alionyesha kuwa nawanafunzi 12 kamati kuu watu ya watatu, kwahiyo Sensa imeendelea kufanyika toka agano la kale adi jipya.

Wananchi kwa nyakati tofauti walisema wapo tayari kuhesabiwa siku ya Sensa tarehe 23 agosti 2022.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa