• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MILIONI KUMI NA MOJA NA LAKI TANO ZATOLEWA NA MBUNGE WA JIMBO LA SONGEA MJINI KUSAIDIA VIKUNDI.

Tarehe ya kuwekwa: May 28th, 2021

 Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Dkt. Damas Ndumbaro  Waziri wa Maliasili na Utalii ametoa fedha kiasi cha shilingi  Milioni kumi na moja na laki tano kwa vikundi 17 ndani ya Halmashauri ya Songea kwa lengo la kuinua vikundi vya wajasiriamali ili kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili katika  wanavikundi hao.

Zoezi hilo limefanyika leo tarehe 28 Mei 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kusimamiwa na  Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano  ambaye alikuwa akimwakilisha  Mbunge  wa Jimbo la Songea Mjini Dkt. Damas Ndumbaro Waziri wa Maliasili na Utalii.

Mbano alisema Manispaa ya Songea ina  jumla ya vikundi 21 vya wajasiliamali   kati ya hivyo vikundi 17 vimewezeshwa kupata mkopo, na vikundi 4 havikukidhi vigezo vinavyokubalika.

Amewataka wajasiriamali waliopokea fedha hizo kuhakikisha wanazitumia matumizi sahihi ili waweze kutatua changamoto zinazowakabili ikiwemo na kukamilisha miradi  iliyoanza kufanyika katika vikundi vyao  na  kuwasaidia kujikwamua kiuchumi wao binafsi na kuleta maendeleo kwenye jamii inayowazunguka. ‘Mbano alisisitiza’.

Naye Mratibu wa vikundi ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Alela Yazidu Kapinga amesema jumla  ya vikundi 17  vyenye jumla ya wanachama 417 wamepokea fedha kutoka kwa Mbunge wa Songea Mjini yenye jumla ya  thamani ya shilingi   milioni kumi na moja na laki tano  kwa wajasiliamali  wanaojishughulisha na  miradi mbalimbali ikiwemo utengenezaji wa bidhaa za  sabuni, ufugaji wa kuku na kilimo.

Kwa nyakati tofauti wakitoa shukrani za dhati  wajasiriamali hao  “walisema wanashukuru kwa msaada uliotolewa na Mbunge  Dkt. Damas Ndumbaro  ambapo wameahidi  kuendeleza miradi ya vikundi  kwa kuwezeshana pamoja na kubuni miradi mingine  mipya yenye tija kwa ajili ya ustawi wa  vikundi vyao.”

Fedha hizo hazijatolewa kama mkopo  na hazina riba, kwa lengo mahususi  la kuwainua wajasiliamali wadogo wadogo  waishio  Songea Mjini.

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA,

28.05.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa