• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI 10 YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BIL. 4 YAFUATILIWA NA TAKUKURU - RUVUMA

Tarehe ya kuwekwa: August 21st, 2023

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma yafanikiwa kufuatilia utekelezaji wa miradi kumi ya maendeleo yenye  thamani ya Bil. 4,977,140,179  katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2023.

Miongoni mwa miradi iliyofuatiliwa ni pamoja na  ujenzi wa miundombinu ya maji katika vijiji vya Wilaya ya Tunduru yenye thamani ya Mil.  2,591,574,071,  miundombinu ya barabara, madarasa  wilaya ya Songea, Nyasa,Tunduru, Namtumbo na Mbinga yenye thamani ya 2,175,566,108 pamoja na ujenzi wa madarasa katika shule za Sekondari katika Wilaya ya Nyasa na Namtumbo yenye thamani ya Mil. 210,000,000.

Hayo yamejiri katika kikao cha TAKUKURU Mkoa kilichofanyika leo tarehe 21 Agosti 2023 katika ofisi ya TAKUKURU na kuhudhuriwa na Waandishi wa Habari Mkoa wa Ruvuma kwa lengo la kutoa taarifa kwa umma ya utendaji kazi wa kipindi cha  April hadi Juni 2023.

Akizungumza Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Hamza Mwenda alisema” katika ufuatiliaji wa miradi hiyo, miradi 5 yenye thamani ya shilingi 3,758,557,179 ilikutwa na mapungufu ambapo hatua mbalimbali zilichukuliwa ili kuondoa mapungufu hayo.”

Mwenda aliongeza kuwa, Kwa upande wa uchunguzi  kumekuwa na malalamiko 28 kati ya malalamiko hayo  malalamiko 16 yamehusishwa  rushwa, katika sekta ya  ardhi malalamiko 6, serikali za mitaa 02, afya 01, fedha 09, manunuzi 01, nishati 04, elimu 03 , na maji 01, pia taarifa  12 hazikuhusishwa rushwa.

Aidha, Kwa upande wa mashtaka alibainisha  kuwa  jumla ya kesi 04 zilifunguliwa ambapo kati ya hizo,   kesi 03 zilikufunguliwa  katika mahakama ya wilaya ya  Songea ambazo zimeisha na Jamhuri ilishinda kesi hizo na kesi 01bado inaendelea katika Mahakama ya wilaya Namtumbo.

TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma inaendelea  kutekeleza  mikakati ya utoaji wa Elimu kwa jamii juu ya Rushwa na madhara yake hususani katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, kwa lengo la kuzuwia mianya ya Rushwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo na Taasis za Umma na Taasis binafsi kwa kushirikiana na vijana wa Skauti kwa dhana ya kujenga uadilifu na uzalendo.  

IMEANDALIWA NA;                                                                                                    

AMINA PILLY;

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.

 




Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa