• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI YA UVIKO 19 KUFIKIA HATUA YA KUEZEKWA NA LIPU MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: November 24th, 2021

Na; 

AMINA PILLY

AFISA HABARI - MANISPAA YA SONGEA.

24.Novemba .2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi Wilbert Ibuge amewataka wataalamu  wa Manispaa ya Songea kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uaminifu, uadilifu na uwazi ili kufanikisha utekelezaji wa miradi inayoendelea kujengwa.

Brigedia Ibuge ametoa pongezi hizo akiwa katika ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya mpango wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 ambayo imefanyika leo tarehe 24 novemba 2021 na kufanikisha kutembelea miradi katika kata ya Mateka, Matogoro, Msamala, Mshangano, Lilambo, Mjimwema, na Lizaboni ambayo ipo hatua ya kuezekwa na lipu.

Alisema  lengo la kutembelea  miradi hiyo  ni kutaka kukagua na kujiridhisha hatua ya utekelezaji wa miradi hiyo na thamani ya fedha iliyotumika  ambapo kwa manispaa ya Songea  inatarajia kukamilisha na kukabidhiwa kwa mkuu wa Wilaya ya Songea ifikapo   tarehe 10 disemba 2021.

Ametoa wito  kwa wafanyabiashara wote Mkoani Ruvuma kuacha kupandisha bei ya vifaa vya ujenzi kwa lengo la kujinufaisha wao bila kujali uzalendo wa Taifa lao kwani Watoto wanaosoma katika shule hizo ni familia zao  pia.

Alisema lengo la Serikali ya awamu ya sita ni kutoa huduma bora kwa wananchi pamoja  na  kutatua changamoto zinazowakabili wananchi ikiwemo na kutoa huduma bora za afya, Elimu, miundombinu bora za barabara, na maji. Alibainisha. 

Kwa upande wa Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko  alisema Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepokea  jumla ya Tshs 2,075,000,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali  ya maendeleo katika sekta ya Elimu miradi 26, na Afya ambapo kwasasa miradi yote ya Elimu (UVIKO 19) imefikia hatua ya kuezekwa na lipu.

Dkt. Sagamiko aliongeza kuwa miongoni mwa mikakati iliyowekwa  ni pamoja na  Kutoa mafunzo elekezi ya usimamizi wa miradi kwa kamati zote za ujenzi kwa kila taasisi, Kufanya kikao na wafanyabiashara ili kuwapatia msimamo wa Halmashauri juu ya uhakika malipo na kwa wakati na kutakiwa  kusambaza vifaa vya ujenzi hadi eneo la mradi kabla ya malipo, na    Kutoa bei elekezi kwa baadhi ya vifaa vya ujenzi kama saruji, bati, tofali na nyinginezo.

Akibainisha  baadhi ya chanagamoto zinazoikabili zoezi hilo ni pamoja na Wafanya biashara kupandisha bei ya vifaa vya ujenzi baada ya kuanza kwa utekelezaji wa miradi kwa bidhaa za tofali ambazo hapo awali kabla ya mradi kuanza ilikuwa ni Tshs. 1500 hadi  1700, pia bidhaa za  bati ilikuwa Tshs. 31,000 kabla ya kuanza kwa mradi na hatimaye ikaongezeka hadi Tshs. 33,000.

Akitoa shukrani za dhati kwa Kwa niaba ya Wananchi wa Manispaa ya Songea, alisema  “kwa namna ya kipekee kabisa tunaishukuru Serikali  ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutupatia fedha za ili kuweza kutekeleza miradi  hii ambayo itasaidia kutatua changamoto zilizokuwa zinaikabili Halmashauri ya Manispaa ya Songea hususani Afya na Elimu.

Kwa upande wa afya Manispaa ya Songea imeanza kutekeleza miradi ya ujenzi wa vituo vya afya vipya  3 vilivyopo kata ya Lilambo, Subira na Msamala ambapo imeanza kujenmgwa na kufikia hatua ya msingi ambapo  miradi hiyo inajengwa kwa fedha za mapato ya ndani.

 

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa