• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA RUVUMA KUENDELEA KUPAMBANA NA UVIKO 19.

Tarehe ya kuwekwa: October 22nd, 2021

NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

22.10.2021

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi Wilbert Ibuge ameongoza kikao cha Tathimini ya utekelezaji wa mpango wa jamii shirikishi na harakishi wa utoaji chanjo ya UVIKO 19 katika Mkoa wa Ruvuma, kikao ambacho kimefanyika leo tarehe 22 Oktoba 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na wakuu wa Wilaya zote, wakurugenzi wa Halmashauri zote, viongozi mbalimbali pamoja na wataalamu wa afya.

Akizungumza katika kikao hicho Ibuge amewapongeza wajumbe wa kamati ya afya ya Mkoa kwa kuelimisha na kuhamasisha jamii kupata chanjo ya UVIKO 19 kwa hiari, na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa katika utekelezaji wa mpango wa chanjo iliyotolewa kwa awamu ya kwanza Jassen&Jassen, ambapo wananchi wenye sifa ya kupata chanjo 44,549 sawa na asilimia 99% waliweza kupatiwa chanjo kati ya wananchi 45,020 waliotakiwa kupatiwa chanjo hiyo.

Aliongeza kuwa Serikali ya Tanzania imepokea chanjo aina ya Sino pharm dozi 1,065,600 kwa lengo la kusambaza katika maeneo yote nchini ambapo Mkoa wa Ruvuma umepokea dozi za Sino pharm 31,291 kwa ajili ya kuendelea na zoezi la kutoa chanjo kwa awamu ya pili.

Amewataka viongozi wa kila Halmashauri na wataalamu wa afya kuhakikisha wanatoa elimu na kuhamasisha jamii kushiriki kwa hiari katika zoezi la utoaji chanjo ya UVIKO 19 kwa awamu ya pili ambayo itaanza kutolewa rasmi kwenye vituo vya afya 298 vilivyopo Mkoani Ruvuma ifikapo tarehe 25 Oktoba 2021.

Pia kila Halmashauri inatakiwa kuhakikisha inasambaza chanjo za Sino pharm katika vituo vyote vinavyotoa chanjo za kawaida ambapo matarajio ya Mkoa ni kumaliza chanjo zilizopokelewa ndani ya siku 28 tangu tarehe 25 Oktoba 2021 ya kuanza zoezi hilo la utoaji chanjo hiyo.”Ibuge alisisitiza”

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mpango wa jamii shirikishi na harakishi wa utoaji wa chanjo ya UVIKO 19 kwa awamu ya kwanza Mratibu huduma za chanjo Mkoa wa Ruvuma Winbroad Mvile amesema kuwa utaratibu wa utoaji wa chanjo ya Sino pharm unatakiwa uzingatie njia zilizotumika katika utekelezaji wa utoaji chanjo ya awamu ya kwanza ili wananchi wengi Zaidi waweze kupata chanjo hiyo.

Alisema kuwa mlengwa wa chanjo ya Sino pharm ni mtu yeyote mwenye umri kuanzia miaka 18 ambapo atatakiwa kuchanjwa mara mbili ili mwili kupata kinga kamili dhidi ya UVIKO 19 ambapo amesisitiza wataalamu wa afya kutoa elimu hii kwa jamii ili kujenga uelewa juu ya matumizi sahihi ya chanjo ya Sino pharm.

Chanjo ya Sino pharm ni salama na ina uwezo wa kusisimua mwili ukatengeneza kinga dhidi ya UVIKO 19 kwa asilimia 95% iwapo mlengwa atakamilisha dozi mbili baada ya siku 21 hadi 28 tangu alipochanjwa dozi ya kwanza.”Mvile alibainisha”

Pia, ameeleza kuwa miongoni mwa faida ya chanjo ya UVIKO 19 ni pamoja na kusaidia kutengeneza kinga dhidi ya virusi vya SARS-CoV-2, kulinda mwili dhidi ya maradhi yanayosabaishwa na UVIKO 19 pamoja na kupunguza uwezekano wa kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo. 

Halmashauri ya Manispaa ya Songea imepokea chanjo ya UVIKO 19 aina ya Sino pharm dozi elfu tano na mia tatu (5300) ambazo zinatarajiwa kuanza kutolewa rasmi katika vituo vyote vya huduma ya afya vinavotoa chanjo nyingine ifikapo tarehe 25 Oktoba 2021.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa