• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA RUVUMA NI WA PILI KITAIFA KWA MIMBA ZA UTOTONI KWA 37%.

Tarehe ya kuwekwa: November 29th, 2023

Serikali imekuwa ikichukuwa juhudi mbalimbali katika kuhakikisha inatokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii ikiwemo na kutunga sheria na miongozo mbalimbali inayotolewa na Serikali, pamoja  na Juhudi hizo, bado kuna matukio mbalimbali yanayotokea katika jamii ambayo yanatakiwa kuzuia.

 Hayo yamejiri wakati wa uzinduzi wa Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili Mkoani Ruvuma yaliyofanyika tarehe 28 Novemba 2023 katika eneo la Soko kuu Songea iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali, wananchi na viongozi kwa lengo la kujenga uelewa  kuhusu ukatili wa kijinsia kama uvunjaji wa haki za binadamu kijamii, kiaifa,  kikanda na kimataifa.

Akizungumza Kaimu Katibu Tawala  Mkoa wa Ruvuma Jeremia Sindoro  ameitaka jamii kutumia vyombo vinavyohusika ikiwemo na madawati ya kijinsia, Ustawi wa jamii na vyombo  katika kutokomeza matukio ya kikatili katika jamii.

Sindoro alisema Mkoa wa Ruvuma ni wa pili kitaifa kwa mimba za utotoni ikiwa ni 37% huku Mkoa wa Songwe ukiwa  nafasi ya kwanza  kwa mimba za utotoni  ambapo amewataka wananchi kuwekeza maadili kwa kufanya mazungumzo na watoto ili kuhakikisha wanatimiza wajibu wao pamoja na ndoto zao  sambamba na mafundisho ya dini.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya jamii Mkoa wa Ruvuma Mariamu Juma amesema lengo la maadhimisho hayo ni kuungana na wadau, kupata nguvu ya pamoja katika kuhimiza na kushawishi jamii  kutokomeza vitendo vya kikatili wa kijinsia ili kufikia usawa wa kijinsia.

Bi Mariamu alibainisha malengo mahususi ni pamoja na kuonyesha mshikamno ulimwenguni kote juu ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake, na kuwaunganisha wadau kwa pamoja ili kuendelea kusisitiza wajibu wao katika kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Kauli mbiu ya mwaka 2023 ni “WEKEZA: KUZUIA UKATILI WA KIJINSIA.” 

IMEANDALIWA NA;                                                                                          

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa