• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA wa Ruvuma ulivyodhamiria kufyekelea mbali changamoto ya KKK katika shule za msingi

Tarehe ya kuwekwa: December 8th, 2018

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Prof.Riziki Shemdoe amesema Mkoa wa Ruvuma umedhamiria kuhakikisha kuwa hadi kufikia mwaka 2020 pasiwepo na mwanafunzi hata mmoja asiyejua Kusoma, Kuandika na Kuhesaba(KKK).

Hayo yamesemwa katika hotuba ya Katibu Tawala huyo,iliyosomwa na Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Ruvuma Edmund Siame kwenye mafunzo ya kuibua na kubadilishana simulizi za mabadiliko,yalioshirikisha Halmashauri zote nane za mkoa wa Ruvuma na kufanyika kwenye ukumbi wa kanisa katoliki Jimbo la Mbinga.

Shemdoe amesisitiza kuwa kuwepo kwa wanafunzi wasiojua KKK ni jambo la aibu hivyo ameagiza kila mmoja awajibike katika nafasi yake ili kuhakikisha azima ya kupunguza na kumaliza changamoto ya KKK inatekelezwa kwa vitendo.

“Wanafunzi wasiojua KKK,waondolewa kwa sababu ni aibu atakwendaje mtoto sekondari bila kujua kusoma na kuandika yaani unakuwa umetengeneza kizungumkuti”,amesisitiza.

Ametoa rai kwa wadau waliopata mafunzo hayo kutengeneza mazingira ya wanafunzi kujua KKK wanapomaliza elimu ya msingi na kusisitiza kuwa ni jambo la ajabu mwanafunzi kumaliza darasa la saba akikosa stadi hizo muhimu.

Ameagiza kuwa serikali ya Mkoa wa Ruvuma inataka wanafunzi wanaomaliza darasa la pili wawe wanajua KKK na kwamba waingie darasa la tatu wakiwa wameimarika kitaaluma na kwamba iwapo mwanafunzi hajui KKK hasiruhusiwe kuendelea na darasa la tatu.

Kwa upande wake Mratibu wa Mpango wa TUSOME PAMOJA katika Mkoa wa Ruvuma Bwana Msabaha amesema hayo ni  mafunzo ya awamu ya pili ya simulizi za mabadiliko ambapo katika awamu ya kwanza maafisa hao walipewa mafunzo ya namna ya kuandaa simulizi za mabadiliko.

Msabaha amesema mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa TUSOME PAMOJA katika maeneo matatu ikiwemo eneo la uboreshaji wa KKK,uboreshaji wa mfumo wa elimu na eneo la ushiriki wa jamii katika elimu.

Hata hivyo amesema Mpango wa TUSOME PAMOJA unakaribia kufikisha mwaka wa tatu wa utekelezaji wake na kwamba imebakia miaka miwili ya utekelezaji na kwamba kuna baadhi ya maeneo ya utekelezaji yamefanyika vizuri,na baadhi ya maeneo yapo katikati na maeneo mengine yapo chini.

“Simulizi za mabadiliko zitasaidia kuleta mabadiliko kutoka eneo moja ambalo utekelezaji haukufanyika vizuri hadi eneo jingine kwa kujifunza  toka Halmashauri moja iliyofanya vizuri kwenda nyingine’’,amesisitiza Msabaha.

Mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Mpango wa TUSOME PAMOJA yanayofanyika kwa siku mbili yanashirikisha maafisa elimu,maafisa habari,wenyeviti wa waratibu,maafisa maendeleo ya jamii na wanahabari.

TUSOME PAMOJA ni Mpango unaofadhiliwa na USAID ambao unafanyiwa majaribio katika mikoa ya Ruvuma,Iringa,Morogoro na Mtwara na unalenga kusaidia kuboresha stadi za ufundishaji na KKK katika shule za msingi.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Desemba 8,2018

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa