• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA RUVUMA WAADHIMISHA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA KWA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA.

Tarehe ya kuwekwa: July 25th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

25 JULAI 2022

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema amewaongoza wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo Julai 25.

Maadhimisho hayo yamefanyika nchi nzima kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ambapo Mkoa wa Ruvuma umeadhimisha kwa kufanya usafi wa mazingira katika eneo la soko la Bombambili lililopo ndani ya Manispaa ya Songea.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Pololet alisema kuwa “Maadhimisho hayo ni kumbukumbu muhimu katika historia ya nchi ya Tanzania ambapo tunawaenzi mashujaa waliojitoa mhanga kupigania haki, uhuru na amani wa Taifa letu”.

Aliongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma umeadhimisha siku hiyo kwa kufanya usafi pamoja na kutembelea eneo la Makumbusho lililopo Manispaa ya Songea katika makaburi ambayo walizikwa mashujaa waliopigana vita vya Majimaji mnamo mwaka 1906 – 1907.’Alibainisha’

Pololet ametoa rai kwa wananchi wote Mkoani Ruvuma kuendelea kulinda Amani ya Taifa la Tanzania pamoja na kuhakikisha wanatunza mazingira yanayowazunguka kwa kudumisha utaratibu uliowekwa na Serikali wa kufanya usafi kwenye maeneo mbalimbali ya umma kila ifikapo tarehe ya mwisho wa kila mwezi.

Naye Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro (MB) ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuendelea kuenzi mashujaa hao kwa kudumisha uzalendo, umoja na mshikamano ili kuchochea amani ndani na nje ya mipaka ya Tanzania. ‘Alisisitiza’

Dkt. Ndumbaro amewataka wananchi wote kushiriki kikamilifu katika zoezi la sensa ya watu na makazi linalotarajiwa kufanyika ifikapo Agost 23 mwaka huu kwa lengo la kupata Takwimu sahihi zitakazosaidia Serikali kupanga mikakati ya kuleta maendeleo kwa wananchi.

Amewahamasisha wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kushiriki katika Tamasha la Majimaji Serebuka linaloendelea kufanyika katika uwanja wa Majimaji uliopo Manispaa ya Songea lenye lengo la kudumisha uzalendo pamoja na urithi wa utamaduni kupitia michezo mbalimbali.

Akizungumza wakati wa zoezi la kufanya usafi katika soko la Bombambili, Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Dkt. Frederick Sagamiko alisema kuwa Manispaa ya Songea imejipanga kuimarisha usafi wa mazingira kwa kuboresha mfumo wa uzoaji taka katika maeneo ya umma ikiwemo na masoko kwa kuanza kutoa mikopo ya usafiri aina ya Toyo kwa vikundi, ambao utatumika kwa ajili ya ukusanyaji wa taka hasa kwenye maeneo yasiyoweza kufikiwa na magari makubwa.

Dkt. Sagamiko ametoa wito kwa wananchi kuunda vikundi vya wajasiriamali kwa kuzingatia makundi maalum (wanawake, vijana na watu wenye ulemavu) ili kuweza kupata fursa za mikopo ambayo itasaidia kukuza uchumi binafsi pamoja na Taifa wa ujumla.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa