• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA RUVUMA WAADHIMISHA SIKU YA MUUNGANO KWA KUSHIRIKI KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA.

Tarehe ya kuwekwa: April 26th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

26.04.2022

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ameongoza wakazi wa Manispaa ya Songea kwenye zoezi la usafi wa mazingira kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ikiwemo na eneo la soko kuu la Manispaa ya Songea pamoja,  Soko la Manzese, pamoja na vituo vya afya.

Tukio hilo limefanyika kufuatia maadhimisho ya siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo mnamo tarehe 26, Aprili ambapo Mkoani Ruvuma siku hii imetumika katika kuchochea jamii kushiriki katika zoezi la usafi wa mazingira.

Akizungumza na wananchi baada ya zoezi la usafi, Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, “amesema kuwa katika maadhimisho haya Mkoa wa Ruvuma umelenga kuchochea uzalendo na utamaduni wa kufanya usafi wa mazingira uliowekwa na Serikali kila ifikapo jumamosi ya mwisho wa mwezi.”

Pololet amewataka wananchi kujenga tabia ya kufanya usafi wa mazingira yanayowazunguka kila siku kwa lengo la kujiepusha na magonjwa mbalimbali pamoja na kuweka Mkoa wa Ruvuma katika hali ya usafi.”Alisisitiza”

Alisema kuwa wajibu wa kuondoa takataka ni jukumu la watu wote ambapo kila mwananchi anatakiwa kushiriki kwa kufuata muongozo uliowekwa na Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuchangia gharama za uzoaji wa takataka kwa kila nyumba.

Ametoa maagizo kwa Afisa mazingira Manispaa ya Songea pamoja na viongozi wa masoko kuhakikisha kuwa kila siku kabla ya kuanza kufanya biashara wafanyabiashara wote waanze kwa kufanya usafi katika maeneo yao.

Aliongeza kuwa kila mwananchi anatakiwa kufanya usafi katika maeneo ya umma ifikapo jumamosi ya mwisho wa mwezi pamoja na kila jumamosi ya mwisho wa wiki kutumika kama siku ya kufanya mazoezi kwa lengo la kuimarisha afya.’Pololet alisisitiza’

Kwa upande wake Afisa Mazingira Manispaa ya Songea Philipo Benno Mpwesa alisema kuwa Manispaa ya Songea ilipokea agizo la kuadhimisha siku hii kwa kufanya usafi wa mazingira kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo zoezi hilo limefanyika katika kila mtaa yote 21 iliyopo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano alieleza kuwa Manispaa ya Songea imejipanga kukabiliana na changamoto ya ongezeko la uzalishwaji taka kwa  kuimarisha mfumo wa uzoaji taka hizo ambapo hadi  kufikia Julai 2022 Halmashauri itaweza kutoa fursa kwa Taasisi binafsi ili kusaidia kusafisha Manispaa ya Songea.

Amewataka kuanzia tarehe 27 Aprili 2022 kila mfanyabiashara mdogo (machinga) kuhakikisha anafanya biashara katika maeneo rasmi yaliyopangwa na Serikali kwa lengo la kuendelea kudhibiti uchafuzi wa mazingira unaotokana na ufanyaji biashara katika maeneo yasiyo rasmi na kukiukwa kwa agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa. “Alisisitiza”

Mwisho.

 

  

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa