• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKOA WA RUVUMA WAKUSUDIA KUCHANJA CHANJO YA POLIO KWA WATOTO WALIO CHINI YA MIAKA MITANO 241,966..

Tarehe ya kuwekwa: May 19th, 2022

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

19 MEI 2022

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema amezindua zoezi la utoaji chanjo ya ugonjwa wa polio awamu ya pili kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Uzinduzi huo umefanyika leo tarehe 19 Mei 2022 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na wakuu wa Wilaya zote Mkoani Ruvuma, wakurugenzi wa Halmashauri, wataalamu wa afya pamoja na viongozi mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Mgema alisema kuwa lengo la utoaji wa chanjo hiyo ni kuongeza kinga ya kuzuia uwezekano wa watoto walio na umri chini ya miaka 5 kupata madhara yatokanayo na virusi vya polio ambapo Mkoani Ruvuma zoezi la utoaji chanjo hiyo limeanza Mei 18 hadi ifikapo Mei 21, 2022.

Amewataka wataalamu wa afya kuhakikisha watoto lengwa wote Mkoani Ruvuma wanapatiwa chanjo hiyo ambayo itatolewa nyumba kwa nyumba, kwenye vituo vya afya 316 Mkoani Ruvuma pamoja na maeneo yenye mikusanyiko ya watoto ikiwemo na mashuleni.

Mgema amewataka wakuu wa Wilaya pamoja na wakurugenzi wa Halmashauri zote kusimamia zoezi la iutoaji chanjo kwa ufanisi ili kuhakikisha watoto wote lengwa Mkoani Ruvuma wanapata chanjo hiyo.

Ametoa rai kwa viongozi wa dini wote kuhamasisha na kutoa elimu kwa jamii kupitia nyumba za ibada kuhusiana na umuhimu wa watoto kupata chanjo hiyo ambayo ni salama na haina madhara yoyote kwa afya ya mtoto .”Alisisitiza”


Naye Mratibu wa huduma za chanjo Mkoa wa Ruvuma Dkt. Winbroad D. Mvile alisema kuwa ugonjwa wa Polio unasababishwa na kirusi cha Polio ambacho huenezwa kwa kula chakula na kunywa maji yaliyochafuliwa na kinyesi cha mtu mwenye ugonjwa huo.

Aliongeza kuwa ugonjwa huo huathiri zaidi watoto wenye umri chini ya miaka 5 ambapo dalili za ugonjwa huo ni pamoja homa, maumivu ya mwili, kichwa na shingo hali inayopelekea kupooza kwa ghafla na hatimaye kifo.


Mvile aliongeza kuwa Mkoa wa Ruvuma umepokea jumla ya chanjo ya Polio Laki 354,000 ambapo kwa awamu ya kwanza ulipokea chanjo Laki 278,000 na kwa awamu ya pili umepokea chanjo Elfu 76000 ambazo zinatarajiwa kutolewa kwa watoto lengwa walio chini ya miaka mitano Laki 241,966  kwa Mkoa wote wa Ruvuma.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa