• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI MANISPAA YA SONGEA AMEONGOZA MAANDAMANO YA SIKU YA WAUGUZI DUNIANI.

Tarehe ya kuwekwa: May 12th, 2021

Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea Tina Sekambo ameongoza Maandamano ya siku ya wauguzi duniani yaliyofanyika katika kituo cha afya Mjimwema Manispaa ya Songea leo tarehe 12.05.2021.

Maadhimisho hayo yameambatana na utoaji wa kiapo kwa wauguzi, utoaji wa zawadi kwa wagonjwa waliolazwa Hosptalini hapo,  ambapo katika maadhimisho hayo yameshirikisha wauguzi kutoka  zahanati zote za Manispaa ya Songea, ngazi ya kliniki, na  vituo vya afya kwa lengo la kukumbushana wajibu na majukumu ya wauguzi ili kuleta mabadiliko chanya katika afya ya jamii.

 Sekambo alianza kwa kuwashukuru wauguzi wote kwa kujitolea  kufanya kazi kwa weledi ikiwemo na kutoa huduma bora kwa jamii sambamba na  kupunguza maambukizi  mapya ya VVU na magonjwa mbalimbali yanayoambukizwa kwa njia ya hewa, kupunguza vifo vya akinamama wajawazito pamoja na watoto wachanga ambapo kwa mwaka  2020 kituo cha afya  Mjimwema akinamama 4984 walijifungua salama.

Miongoni mwa changamoto ambazo ameahidi kuzifanyia kazi  ni pamoja na ukosefu wa vitendea kazi,  ukosefu  wa gari la kubebea wagonjwa (AMBULANCE) wanapopata rufaa ya kwenda hospitali nyingine, upungufu wa wauguzi ambapo Manispaa ya Songea inapaswa kuwa na wauguzi 233 lakini hadi sasa kituo kina  wauguzi  91 sawa na asilimia 39% hivyo kuna upiunguzfu wa wauguzi 142 sawa na asilimia 60%.  

Amemuagiza Afisa utumishi Manispaa ya Songea  kutembelea kituo cha afya Mjimwema kwa ajili ya kusikiliza kero na  kutoa elimu kwa wauguzi  kuhusiana na masuala ya kiutawala, utumishi na maslahi ya watumishi wa kada ya Afya ‘Sekambo alibainisha’.

Naye  Afisa muuguzi msaidizi Manispaa ya Songea Rhoda Mtung’e  ametoa ombi  kwa serikali  kuendelea kutoa ajira kwa wauguzi wanaohitimu ili kupunguza au kuziba pengo la upungufu wa wauguzi katika Manispaa ya Songea pamoja na  kuongeza vitendea kazi vya kutosha katika vituo vya afya ambavyo vinaupungufu ili kusaidia kupunguza vifo na malalamiko kutoka kwa wateja.

Mtung’e alisema lengo la kutoa  kiapo kwa wauguzi ni kufanya kazi kwa uadilifu ikiwemo na kutotoa siri za wagonjwa, kutotoa au kupokea rushwa   pamoja na kuzingatia misingi na maadili ya uuguzi kwa jamii.

Kauli mbiu ya siku ya wauguzi duniani mwaka 2021 ni “WAUGUZI SAUTI INAYOONGOZA DIRA YA HUDUMA YA AFYA”.

 

IMEANDALIWA NA,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA,

12.05.2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa