• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkurugenzi Manispaa ya Songea Wakili. Muhoja, Akabidhi Eneo la Mradi wa Ujenzi wa masoko na Kiwanda Lilambo.

Tarehe ya kuwekwa: July 15th, 2025

Na; Amina Pilly;

Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea, Wakili Bashir Muhoja, leo tarehe 15 Julai 2025 amekabidhi rasmi eneo la mradi wa ujenzi wa Soko la Kisasa katika maeneo ya Manzese A & B pamoja na kiwanda cha kuchakata mazao ya nafaka kilichopo Kata ya Lilambo kwa Mhandisi kutoka Kampuni ya China National Aero Technology International Engineering Cooperation.

Picha ya eneo la Soko la Manzese A kabla ya kuanza ujenzi.

Picha ya Eneo la Soko la Manzese B kabla ya kuanza ujenzi.

Mradi huo mkubwa unaogharimu jumla ya Shilingi Bilioni 22.9, unatarajiwa kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo na biashara katika Manispaa ya Songea kwa kuongeza thamani ya mazao, kukuza uchumi wa ndani, na kutoa ajira kwa wananchi wa maeneo husika.

Akizungumza wakati wa  makabidhiano hayo, Mkurugenzi Muhoja alimtaka Mhandisi anayesimamia mradi huo kuhakikisha anafanya kazi kwa uweledi wa hali ya juu, uwajibikaji, na kuzingatia muda uliopangwa. Pia alisisitiza umuhimu wa kuwa na mipango madhubuti ya kazi hususan katika kuzingatia msimu wa mvua unaokuja, ili mradi usikwame wala kucheleweshwa.

“Ninamtaka Mhandisi ahakikishe kazi hii inafanyika kwa viwango vya juu, kwa uadilifu, na kwa kuzingatia muda. Tunahitaji kuona tija kwa wananchi wetu, na hatutakuwa tayari kuona ucheleweshaji wowote unaotokana na kutozingatia hali ya hewa au maandalizi duni,” alisema Muhoja.

Kwa upande wake, mhandisi wa  kampuni hiyo aliahidi kutekeleza mradi huo kwa kuzingatia viwango vya kimataifa na kuhakikisha unakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa.


Makabidhiano hayo yamepokelewa kwa matumaini makubwa na wananchi, ambapo wengi wameeleza kuwa mradi huo utasaidia kuboresha miundombinu ya masoko na kuimarisha mnyororo wa thamani wa mazao ya kilimo kwa wakulima wa maeneo hayo.

Ujenzi unatarajiwa kuanza rasmi katika kipindi kifupi kijacho mara baada ya maandalizi ya awali kukamilika

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA July 08, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 July 04, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi Manispaa ya Songea Wakili. Muhoja, Akabidhi Eneo la Mradi wa Ujenzi wa masoko na Kiwanda Lilambo.

    July 15, 2025
  • Bil. 22.9 Kujenga Masoko ya Kisasa Manzese A na B, na Kiwanda cha Kuchakata Mazao ya Nafaka Lilambo

    July 06, 2025
  • MBUNGE SONGEA MJINI AKABIDHI KOMPYUTA NA KUFADHILI UKARABATI WA OFISI ZA POLISI

    June 27, 2025
  • DC Songea bAzindua Dawati la Huduma za Ustawi wa Jamii Stendi ya Mabasi Songea

    June 24, 2025
  • Tazama zote

Video

UJENZI WA MASOKO MANZESE A & B, NA KIWANDA KUANZA KUJENGWA
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa