• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKURUGENZI Manispaa ya Songea awaagiza wakuu wa Idara kusimamia mapato

Tarehe ya kuwekwa: September 23rd, 2018

MKURUGENZI wa Hamashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Tina Sekambo amefanya vikao siku tatu mfululizo na wakuu wa Idara na vitengo pamoja na wakusanyaji wa mapato kwa kutumia mashine yaani POS lengo likiwa ni kuweka mikakati mizito ya kuhakikisha mapato ya Halmashauri hiyo yanakusanywa kwa usimamizi wa kutosha ili kuhakikisha hakuna mapato yanayopotea au kuvuja.

Sekambo ameamua kufanya vikao hivyo kufuatia mapato ya Halmashauri kuonekana yameshuka katika mwezi huu hivyo ameagiza kila Mkuu wa Idara na vitengo vinavyohusika na ukusanyaji wa mapato kusimamia POS zote ili kuhakikisha kuwa mapato ya Halmashauri hiyo yanapanda.

Sekambo ameagiza kitengo cha TEHAMA,,watendaji wa mapato na Idara ya fedha sasa kufanyakazi kwa pamoja yaani Team work ili kuhakikisha POS zote zinakusanya mapato wakati wote na kwamba pasiwepo na kisingizio cha POS kuharibika au kupotea ambapo ameagiza yeyote ambaye atafanya uzembe wa aina yeyote hata sita kuchukua hatua za kisheria ikiwepo kulipa fedha zote ambazo zitakuwa zimepotea kwa uzembe.

Amewataka wakusanyaji hao kwenda kila mahali ambako wafanyabiashara wameweka bidhaa zao kwenda kukusanya mapato ambapo ameagiza kila Mkuu wa Idara kutambua POS zake na kiasi cha fedha ambazo zinakusanywa kwa siku kuhakikisha zinaingia katika Halmashauri na kwamba siku ya Alhamisi ambayo ni maalum kwa ukaguzi wa POS kila mkuu wa idara asimamie na kuhakikisha fedha zinapelekwa Benki.

"Wote mnaotumia POS hakikisheni mnafuata maelekezo ambayo mlipewa kabla ya kuanza kazi ,ikiwemo kutozima data za POS  na kuacha kubonyesha mara mbili mashine ya print ambayo itasoma mara mbili,kuanzia sasa mkusanyaji yeyote ambaye atabonyesha mara mbili POS yake atalipia gharama hiyo,fuata ulichofundishwa kabla ya kuanza kutumia mashine uliopewa'',alisisitiza Sekambo.

Hata hivyo amesema wakusanyaji wote wanaodaiwa wanatakiwa kurudisha fedha hizo ambapo wataalam wa Manispaa yaani CMT wametoa hadi Oktoba 4 mwaka huu wakusanyaji wote wanaodaiwa na Halmashauri wawe wamelipa madeni yao na kwamba kuanzia sasa Halmashauri itaanza kuchukua hatua kwa wanaoisababishia Halmashauri hasara ikiwemo kuwaondoa katika kazi ya ukusanyaji wa mapato na kulipa fedha wanazodaiwa.Halmashauri ya Manispa ya Songea imenunua POS zaidi ya 100.

Imeandaliwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Septemba 23,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa