• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Apongeza kwa Utekelezaji wa Miradi

Tarehe ya kuwekwa: May 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Duka la Dawa linalojengwa katika Kituo cha Afya Mjimwema, Manispaa ya Songea, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe hilo la msingi, Kanali Ahmed ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuibua na kutekeleza mradi huo muhimu unaolenga kusogeza huduma za afya karibu zaidi na wananchi.

“Kunapokuwa na huduma zinazofikiriwa kutolewa kwa wananchi, ni lazima zikamilike kwa wakati ili waweze kunufaika na huduma hizo,” alisema Kanali Ahmed.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kukamilika kwa wakati kwa mradi huo, hasa ikizingatiwa kuwa unatarajiwa kuzinduliwa rasmi kupitia Mbio za Mwenge wa Uhuru.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa alitembelea pia mradi wa ujenzi wa Maegesho ya Malori katika Kata ya Lilambo na kueleza kuridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wake. Alitoa wito kwa viongozi wa maeneo husika kuendelea kushirikiana na Serikali ili miradi hiyo ianze kuleta mapato yatakayowezesha maendeleo kwa maeneo mengine.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mjimwema, Bi. Alice Kitindi, alisema kuwa mradi huo ulianzishwa na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Songea tarehe 6 Januari 2025 na unatarajiwa kukamilika tarehe 6 Mei 2025, ukiwa na unalenga  kupunguza umbali wa wananchi kufuata huduma za dawa.

Bi. Kitindi alieleza kuwa hadi sasa ujenzi huo umefikia asilimia 99 ya utekelezaji, ambapo umegharimu shilingi 72,389,742/= licha ya makadirio ya awali kuwa shilingi 68,674,652.50.

Naye Diwani wa Kata ya Mjimwema, Mhe. Sylivesta Mhagama, alibainisha kuwa mradi huo unatekelezwa kwa kutumia fedha za mapato ya ndani, na ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha kuwa changamoto ya upatikanaji wa huduma ya dawa kwa wananchi wa kata hiyo inatatuliwa kwa haraka na ufanisi.

Na;

AMINA PILLY 

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Apongeza kwa Utekelezaji wa Miradi

    May 05, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Awataka Waajiri kuzingatia Misingi ya Utawala Bora

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Songea Akizindua Stendi ya Bajaji - Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa