• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma azindua kampeni ya uhamasishaji watumishi kutumia TTCL

Tarehe ya kuwekwa: June 25th, 2019

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme amezindua kampeni ya watumishi wa umma kujiunga na mtandao wa TTCL kwenye ukumbi wa sekondari ya Songea Girls mjini Songea.

Akizungumza kabla ya uzinduzi huo,Mndeme alisema ni muhimu kwa watumishi wa umma kutumia mtandao wa TTCL ili waweze kujiimarisha kwa kupanua huduma na kuzalisha faida.

Amesema TTCL imekuwa inatoa gawio kwa serikali na kwamba Rais Dkt.John Magufuli huitumia faida inayotolewa na TTCL katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania.

Amesema serikali ya Awamu ya Tano imekusudia kuliimarisha Shirika la TTCL na kwamba shirika hilo ni nembo pekee ya kumkumbuka baba wa Taifa ndiyo maana linatakiwa kuimarishwa kwa  Taasisi za serikali kwa kutumia huduma zake katika shughuli za mawasiliano.

“Serikali hii inatambua mchango wa mawasiliano na Shirika la Mawasiliano la Tanzania katika kuleta maendeleo yanayofikia na uchumi wa viwanda,mawasiliano ni muhimu sana katika kukuza uchumi kupitia simu za mezani,mkononi,intaneti na data’’,alisisitiza.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ameagiza Taasisi zote za serikali zilizopo katika Mkoa wa Ruvuma ambazo hazijaanza kutumia laini za mtandao wa TTCL kwa ajili ya mawasiliano zianze mara moja.

Amewaagiza viongozi wa serikali katika Mkoa ,wanaolipwa vocha za mawasiliano na serikali,watumie laini za TTCL na kwamba lengo la serikali sio kuwazuia watu kutumia mitandao mingine bali ni kuimarisha TTCL ambacho ndiyo chombo cha mawasiliano cha serikali.

“Wakati sasa umefika sasa watumishi wa umma kuunga mkono juhudi za serikali za kuimarisha mtandao wa TTCL kwa manufaa ya uchumi wa nchi yetu’’,alisisitiza Mndeme.

Meneja wa TTCL Mkoa wa Ruvuma Zabron Magabula amesema idadi ya watumiaji wa mtandao wa TTCL ni ndogo ambapo kutokana na mfumo wa usajili wa watumishi wa umma kuna jumla ya watumishi 102 katika Mkoa wa Ruvuma.

Amesema kati ya watumishi hao Manispaa ya Songea watumishi 38,Songea vijijini 26,Tnuduru 24,Mbinga 12 na Nyasa sita na kwamba idadi hiyo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya watumishi wa umma waliopo mkoani Ruvuma.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa