• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma azindua kongamano la walimu na NMB

Tarehe ya kuwekwa: August 28th, 2019

BENKI ya NMB imedhamiria katika kutoa huduma za kibenki za kidigitali kwa watanzania wote  ili kuweza kufanya miamala na malipo mbalimbali kwa ufanisi na kasi zaidi.

Akizungumza katika kongamano la  walimu na  NMB  Wilayani ya Songea mkoani Ruvuma lililofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea,Afisa Mwandamizi wa Amana za wateja binafsi kutoka NMB Makao makuu, Isaack Mgwassa anasema njia hiyo ni bora zaidi na inaendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia ambayo itasaidia kuleta mwamko mkubwa kwa watanzania.

 “NMB imeona ni muhimu kukutana na wadau wake wakubwa katika huduma za kibenki hivyo imetenga siku maalum ya kuzungumza na wateja na kuwapa maendeleo ya benki yao na huduma mbalimbali zinazotolewa ili kuwapa uelewa zaidi’’,anasema Mgwassa.

Anasema kupitia kongamano la  walimu watapata mrejesho na mawazo mbalimbali kuhusiana na huduma za NMB ambayo yatasaidia kufanya maboresho.

Anasema NMB inaamini kupitia  waratibu Elimu Kata na  walimu wakuu katika shule za msingi na sekondari katika Wilaya ya Songea,watasaidia kupeleka elimu watakayoipata kwa walimu wenzao na jamii yote kwa ujumla kuhusiana na huduma bora  za NMB  zinazomgusa kila Mtanzania.

Hata hivyo anasema  utafiti umebaini kuwa licha ya watanzania kufikia zaidi ya milioni 50,ni asilimia chini ya 40 tu ndiyo wenye akaunti benki na kwamba zaidi ya asilimia 60 ya watanzania wanamiliki simu za mkononi na wana uwezo wa kufanya malipo na miamala kupitia simu za mkononi.

Kulingana na Meneja Mwandamizi huyo,NMB katika nchi nzima ina wateja zaidi ya milioni 3.2 kati yao zaidi ya wateja milioni 2.5 wanatumia simu kufanya miamala,kuangalia salio,kufanya malipo mbalimbali,kulipia umeme na kodi mbalimbali.

“Tumedhamiria kuona NMB inakuwa Benki ya kwanza Tanzania kuanzisha mfumo wa kutotumia fedha unapokuwa kwenye shughuli zako bali kutumia kadi na simu za mikononi kufanya manunuzi na matumizi mengine ya fedha  zako zilizopo Benki’’,anasisitiza Mgwassa.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro akizungumza kabla ya kufungua kongamano hilo ametoa rai kwa NMB kuendelea kutoa elimu ya huduma za kibenki kutokana na takwimu kuonesha ni chini ya asilimia 40 ya watanzania  ndiyo wenye akaunti benki.

“Kuna kila sababu ya vyombo vya fedha kuwa na program maalum ya kutoa elimu hasa katika maeneo ya vijijini ili waweze kupata elimu sahihi na kufaidika na huduma za kifedha zinazotolewa na benki hapa Tanzania’’,anasema Mndeme.

Mndeme ameipongeza NMB kwa kutoa mikopo mingi kwa wafanyakazi wa serikali kuu na serikali za mitaa na kwamba asilimia kubwa ya walimu hapa nchini wamefaidika na mikopo ya benki hiyo.

Takwimu  za Benki ya NMB zinaonesha kuwa hadi sasa imetoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni mbili ikiwa ni mikopo kwa wafanyakazi kiwango ambacho amesema ni kukubwa kuwahi kutolewa na Taasisi za kifedha nchini.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa NMB kuendelea kuandaa program nyingi kwa watumishi wote wa serikali ili kuwapatia fursa ya kujua huduma zinazotolewa na Benki na kuendelea kubuni bidhaa mbalimbali za kibenki ambazo mtumishi wa kawaida anaweza kumudu.

“Endeleeni kupanua wigo wa mikopo,na mikopo yenu iwe na riba nafuu,pia endeleeni kuboresha huduma kwa wateja ili idadi yao iweze kuongezeka na kupata fursa nyingi za kukopo kwa masharti nafuu na kuongeza tija kwenye maeneo yao ya kazi’’,anasisitiza Mndeme.

Daniel Zake ni Meneja wa NMB tawi la Songea akitoa shukrani za NMB kwa mgeni rasmi, ameeleza kuwa Benki hiyo ina matawi  223 nchi nzima,ATM zaidi ya 800 na wakala zaidi ya 7000 ambapo anasema Benki hiyo ni sikivu ipo tayari kusikiliza changamoto za wateja kama walimu na kuzitafutia ufumbuzi.

Zake amemthibitishia Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kuwa suala la riba litafanyiwa kazi na uongozi wa NMB na kwamba kwa kanuni za benki kuna vikao mahususi kwa ajili ya kupitisha vitu vya namna hiyo.

Naye Mwakilishi wa Afisa Elimu Mkoa wa Ruvuma Musa Musa anasema Benki  ya NMB ni nguzo muhimu kwa watumishi wa umma wakiwemo walimu kwa sababu imekuwa inatoa mikopo mbalimbali kwa riba nafuu hali ambayo imesababisha walimu wengi kujenga nyumba,kusoma na kusomesha watoto wao katika ngazi mbalimbali za elimu.

Ametoa rai kwa walimu na watanzania wengine kwa ujumla kuendelea kutumia huduma zinazotolewa na Benki ya NMB  kutokana na huduma zake kuwa bora,usalama na uhakika.

Jane Nyandindi ni Mkuu wa shule ya sekondari ya Lukala katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea ambaye ni mmoja wa wateja wa Benki ya NMB, anasema amefurahishwa na  kongamano la walimu na NMB ambapo kupitia hafla hiyo, wamepata mwanga wa kutosha kuhusiana na huduma mbalimbali za NMB.

Nyandindi anasema amekuwa mteja wa NMB tangu mwaka 1999 na kwamba tangu wakati huo amenufaida na mikopo ya benki kwa watumishi ambayo imemsaidia kupata maendeleo mbalimbali.

Vitus Ngoma ni Mkuu wa shule ya msingi Mashujaa katika Manispaa ya Songea anasema kongamano la NMB limemwezesha kutambua kwa kina huduma mbalimbali za Benki ya NMB.

Anasema tangu amekuwa mteja wa NMB ananufaika na huduma mbalimbali zikiwemo kupokelea mshahara,kupata mikopo na kwamba huduma karibu zote zinazotolewa ndani ya benki hiyo zinawaridhisha wateja wake.

Hata hivyo ametoa rai kwa Benki  hiyo kuboresha kipengele cha mikopo ili kupunguza riba kwa wateja ambacho kinaleta changamoto kwa watumishi .

 Kongamano hilo  limewashirikisha  walimu wakuu,waratibu elimu Kata na watendaji waandamizi wa elimu kutoka Wilaya Songea zaidi ya 230

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Apongeza kwa Utekelezaji wa Miradi

    May 05, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Awataka Waajiri kuzingatia Misingi ya Utawala Bora

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Songea Akizindua Stendi ya Bajaji - Songea
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa