• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Atoa Wito kwa Wataalamu Kushirikisha Jamii Katika Maamuzi

Tarehe ya kuwekwa: April 15th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewataka wataalamu wa sekta mbalimbali kuwa na utamaduni wa kuishirikisha jamii pamoja na wadau wakati wa kufanya maamuzi yanayohusu maendeleo ya wananchi.

Akizungumza wakati wa ziara yake tarehe 14 Aprili 2025 katika Manispaa ya Songea, Kanali Ahmed alisisitiza umuhimu wa kuwepo kwa vikao vya ushirikishwaji kabla ya kutoa maagizo au kufanya maamuzi muhimu.

"Mnapotaka kutoa maagizo, hakikisheni mnaweka vikao vya kushirikisha jamii juu ya jambo husika, hii itasaidia kutoa elimu kuhusu fursa zilizopo na kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu maendeleo yanayofanywa na Serikali yao," alisema.

Katika ziara hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa alitembelea maeneo ya Stendi ya Ruhuwiko na Mfaranyaki ambapo alisikiliza changamoto mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara na wananchi ambapo alibainisha kuwa Serikali inafanya jitihada kubwa katika kuboresha huduma kwa wananchi, ikiwemo  na kutekelezwa kwa miradi mikubwa ya maendeleo kama ikiwemo na Mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya Shilingi Bilioni 145, Ujenzi wa barabara ya mchepuko (Bypass) ya Songea pamoja na Ujenzi wa masoko 2 ya  Manzese

Kanali Ahmed alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliahidi kutatua tatizo la msongamano wa magari makubwa (maroli) katika mji wa Songea, ambapo alithibitisha kuwa fedha za ujenzi wa barabara ya mchepuko zimeshapokelewa na maandalizi ya kuanza ujenzi huo yako tayari.

Akizungumzia suala la usalama wa wasafirishaji wa bodaboda na bajaji, alieleza umuhimu wa kuwa na sare maalum kwa ajili ya utambulisho wa madereva hao. "Ni muhimu madereva wa bodaboda na bajaji wawe na sare ili waweze kutambulika kirahisi hasa wanapopata matatizo au kutambulika wanapofanya kazi  na Hii pia itasaidia kupunguza athari kutoka kwa maroli na mabasi," alisema.

Katika hatua ya awali, tayari sare 300 za kuakisi mwanga (reflector jackets) zimepatikana kwa ajili ya kugawiwa kwa madereva hao.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea, Michael Mbano, alieleza kuwa Serikali imetekeleza agizo la Rais kwa kutenga eneo maalumu la Wamachinga katika eneo la Majengo, Hata hivyo, bado baadhi yao hawajaanza kulitumia.

"Tunatoa wito kwa wafanyabiashara ambao hawajapata maeneo wafike ofisini kwa Mstahiki Meya ili waweze kupewa nafasi ya kufanyia biashara zao kihalali," alisema Mbano.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi kuwa wavumilivu wakati Serikali ikijiandaa kuanza rasmi ujenzi wa soko la Manzese, ambapo taratibu zote muhimu tayari zimekamilika na utekelezaji wake unatarajiwa kuanza hivi karibuni.

Kwa upande wa wafanyabiashara hao waliishukuru viongozi hao kwa kuwatembelea na kubaini chanmgamoto zinazowakabili ambapo Serikali imeahidi kuzitatua.

IMEANDALIWA NA 

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI.            

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa