• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA WILAYA YA SONGEA "ASISITIZA UBORESHAJI WA TIMU YA MAJIMAJI.

Tarehe ya kuwekwa: January 8th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema ameawataka Wakurugenzi wa Halmashauri wenye miradi ya ujenzi wa madarasa kuhakikisha inakamilika kwa wakati kabla ya kufunguliwa kwa shule januari 11.2021.

Pololet ametoa agizo akiwa katika kikao cha kamati ya  Ushauri  Wilaya DCC, ambacho hushirikisha Wataalamu wa Halmashauri tatu ikiwemo na  Madaba, Halmashauri ya Wilaya ya Songea,  Manispaa ya Songea pamoja na Wadau mbalimbali wa Maendeleo kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea jana 07 januari 2021.

Alisema lengo la kikao hicho ni kupokea ushauri mbalimbali kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi na kusaidia  kuijenga Serikali yetu ili  kuleta Mafanikio yenye tija kwa jamii ya Songea, na kupokea taarifa za utekelezaji wa miradi katika kipindi cha 2019/2020.

Aliongeza kuwa, Serikali imeweka uwekezaji wa kituo kikuu cha mabasi Tanga  kwa ajili ya kuongeza mapato na kugawa fulsa kwa  wananchi wa  Songea hususani wafanyabiashara kwa lengo la kuwainua kiuchumi.

Alisema “mabadiliko yoyote yanagharama pia lazima tutambue kuwa mabadiliko haya yanaleta fulsa kubwa ya kuendeleza mji wa Tanga na fulsa kwa wafanyabiashara , mama lishe, Bodaboda na wengineo kwahiyo msione kama ni jambo la ajabu au kwa ajili ya kuwanyanyasa wananchi hapana.” Nanukuu “Serikali inayoongozwa na Mh. Rais John Pombe Magufuli haipo tayari kuona wananchi wake wananyanyaswa “ Pololet alibainisha.

 

Amewataka wataalamu wa Manispaa ya Songea kuhakikisha stendi ndogo ya Ruhuwiko inaboreshwa haraka iwezekanavyo ili magari yaweze kuingia na kutoka kwa urahisi na usalama Zaidi.

Alitoa wito kwa wasimamizi wa vyombo vya moto ( usalama barabarani)  kuhakikisha wanaimarisha ulinzi na usalama pamoja na kufanya uchunguzi kwa madereva wa boda boda ambao wanajihusisha kuwasafirisha abiria kwa kuwatoza nauli  kubwa  zaidi ya shilingi 15,000  kutoka mjini hadi Tanga kinyume na sheria, endapo watabainika wachukuliwe hatua za kisheria. Pololet ameagiza.

Alisema  Serikali imetoa Tsh bilioni 6.8 kwa ajili ya ujenzi wa stendi ili iwanufaishe wananchi kwa ajili ya ya kuwaletea maendeleo yao  kwahiyo stendi  nilazima itumike ipasavyo. 

 

Akiwahimiza wataalamu hao kila waaandaapo taarifa zao lazima iwekwe taarifa za mikopo iliyotolewa kwa kila kikundi   ili kila  mwananchi apate kufahamu serikali inawafanyia nini  kwa kuzingatia ugawaji sahihi wa  mikopo  ili fedha zinazotolewa na Halmshauri ziwafikie  walengwa kama vikundi vya wananawake 40%, vikundi vya Vijana 40%, na walemavu 20% Kwa ajili ya kuleta chachu ya Maendeleo kwa wananchi pamoja na uboreshaji wa  huduma za afya kupitia vituo vya Afya.

 Akizungumzia timu ya Maji maji ambapo alisema  Zaidi ya miaka minne timu ya majimaji haijacheza ligi kuu ya Tanzania kutokana na kushuka kwa daraja, kutokana na tatizo hilo serikali imejipanga kuboresha timu ya majimaji kwa kuiongezea nguvu ikiwemo na kuchukua changamoto zao kuzipeleka ngazi ya mkoa ili timu hii itazamwe kimkoa Zaidi.

Naye Afisa misitu Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Chale alisema Jiolojia ni muonekanao wa kijiografia wa sehemu Fulani ambayo inahusisha miinuko, miamba, mabonde, mapango na maporomoko.

Chale aliongeza kuwa hifadhi ya jiolojia katika safu yamlima matogoro ipo chini ya usimamizi wa TFS, Serikali ya vijiji pamoja na Taasis zinazojihusisha uhifadhi wa milima ya matogoro kusini, milima ya matogoro mashariki, magharibi, mapambo yamlima matogoro  A na Chandamali, utamaduni wa jamii wa wangoni na wandendeule, makumbusho tatu zilizoko Manispaa ya Songea, mabwawa ya umeme wa maji chipole, maporomoko ya maji nakatuta, msitu wa Chandamali, Mabwawa ya Soamaki Ruhila, na milima ya limamu na mpiganjuchi.

Alisema umuhimu wa kuhifadhi katika safu ya milima ya matogoro ni mkubwa kwa kuwa una vitu vingi vya umuhimu kwa ajili ya kizazi cha leo na kesho pia milima ya matogoro inatarajiwa kuwa nyenzo muhimu kwa kukuza pato la Wilaya na Mkoa kwa kuongeza idadi ya watalii watakaotembelea hifadhi kwa kuongeza vivutio vya watalii. Pia watasaidaia watalii hao kununua vifaa vya kiutamaduni na kusaidia jamii kujiongezea kipato.

 

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

08.Januari 2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa