• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Kapenjama Ndile, Apongezwa Kwa Kuimarisha Uchanjaji wa Chanjo ya Kichaa cha Mbwa

Tarehe ya kuwekwa: September 12th, 2024

Songea Mjini, tarehe 12 Septemba 2024 Mkuu wa Wilaya ya Songea, Kapenjama Ndile, amewapongeza wananchi wa Songea Mjini kwa kujitokeza kwa wingi na kupeleka mbwa wao katika maadhimisho ya uchanjaji wa chanjo ya kichaa cha mbwa. Maadhimisho hayo yalifanyika katika viwanja vya shule ya sekondari Matarawe, Songea Mjini.

Ndile amesisitiza umuhimu wa chanjo hiyo katika kuzuia hatari ya kichaa cha mbwa na kuwasihi wale ambao hawakupata nafasi ya kuchanja mbwa wao kujitahidi kuhakikisha mchakato huo unakamilika. "Chanjo ni muhimu kwa usalama wa jamii, hivyo ni lazima kuhakikisha kuwa mbwa wote wanapewa chanjo ili kupunguza hatari ya ugonjwa huu," alisema Ndile.

Aidha, Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi kutunza mbwa wao kwa njia ya kisasa, ikiwa ni pamoja na kuwajengea mabanda ya kisasa, kuwafungia wakati wa mchana, na kuwaweka katika mazingira bora kwa kuwapa chakula chakutosha. "Hii itasaidia kuboresha hali ya mbwa na kuhakikisha wanakuwa na afya njema," aliongeza Ndile.

Kwa upande wake, Daktari wa Mifugo, Seria Masole Shonyera, ameipongeza serikali kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea katika uratibu wa zoezi hili la chanjo. Shonyera alisema kuwa chanjo ya bure iliyoandaliwa imewezesha kufanikisha uzinduzi wa maadhimisho haya na kutoa msaada mkubwa kwa jamii.

Maadhimisho haya ya kichaa cha mbwa duniani yanafanyika kila mwaka tarehe 28/09, lakini kwa wilaya ya Songea Mjini, yamefanyika mapema mwaka huu kutokana na shughuli nyingine zinazotarajiwa kufanyika katika tarehe hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa