• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilaman Kapenjama Ndile, Akutana na Wafanyabiashara wa Pembejeo Kuangalia Changamoto na Mikakati ya Maendeleo

Tarehe ya kuwekwa: September 14th, 2024


Katika juhudi za kuboresha sekta ya pembejeo na kilimo, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilaman Kapenjama Ndile, leo ameongoza mkutano wa muhimu uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ambapo Mkutano huu uliwaleta pamoja wafanyabiashara wa pembejeo, wakulima, na maafisa wa serikali kwa ajili ya kujadili changamoto na mikakati ya kuimarisha sekta hiyo.

Katika hotuba yake, Mheshimiwa Ndile alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya serikali na wafanyabiashara katika kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo bora kwa wakulima pia Alieleza kuwa serikali imejitolea kuboresha mifumo ya usambazaji na udhibiti wa ubora wa pembejeo ili kuondoa changamoto za ucheleweshaji na ubora wa bidhaa zinazopatikana sokoni.

"Ubora wa pembejeo ni suala la msingi ambalo linahitaji umakini wa hali ya juu, pia Tunahitaji kuhakikisha kwamba pembejeo zinazouzwa zinakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na mamlaka husika," alisema Mheshimiwa Ndile.

 Aliongeza kuwa serikali itatekeleza mfumo madhubuti wa ukaguzi wa ubora wa pembejeo na kuimarisha udhibiti wa bei ili kuhakikisha bei za pembejeo zinakuwa rafiki kwa wakulima.

Wafanyabiashara walipokea mwito wa Mheshimiwa Ndile kwa mikono miwili na walionesha kujitolea katika kuhakikisha kuwa huduma zao zinakidhi viwango vya ubora na bei zinazokubalika pia Walisema watashirikiana na serikali katika kuboresha mifumo ya usambazaji na kutoa mapendekezo kuhusu changamoto wanazokumbana nazo.

Mkutano huu pia uliwashirikisha wafanyabiashara katika kujadili masuala ya bei, ubora wa pembejeo, na ushirikiano wa mawasiliano kati ya pande zote ambapo Viongozi wa serikali walipokea maoni na mapendekezo kutoka kwa wafanyabiashara na wakulima kwa lengo la kutatua changamoto zinazojitokeza.

Mkuu wa Wilaya alimalizia kwa kutoa shukrani kwa washiriki wote na kuwatia moyo kuendelea na juhudi zao za kuboresha sekta ya pembejeo pia alisisitiza kwamba kwa ushirikiano wa karibu, changamoto zitakazokabiliwa zinaweza kutatuliwa kwa ufanisi na maendeleo ya sekta hiyo yataimarika.

AMINA PILLY

KITENGO CHA MAWASILIANO 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa