• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MRADI WA REA AWAMU YA 3 KUTATUA CHANGAMOTO YA UMEME WILAYA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: November 16th, 2021

Na,

AMINA PILLY,

AFISA HABARI MANISPAA.

16.11.2021

Wilaya ya Songea kuanza utekelezaji wa mradi wa REA kwa awamu ya tatu mzunguko wa pili ili kufikia maeneo ambayo bado hayajapata huduma ya umeme.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Kamando Mgema wakati akiongoza kikao kazi cha kamati ya ushauri ya Wilaya ya Songea hapo jana tarehe 15 Novemba 2021, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wa kamati hiyo wakiwemo wakurugenzi wa Halmashauri kutoka Manispaa ya Songea, Madaba na Wilaya ya Songea.

Mgema alisema kuwa Serikali imejipanga kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Wilaya ya Songea kwa kuhakikisha wanapeleka huduma muhimu kwa wananchi katika maeneo mbalimbali hasa maeneo yaliyopo vijijini ikiwemo na miundombinu ya umeme, maji, elimu na afya.

Aliongeza kuwa wataalamu wanatakiwa kutimiza wajibu kwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao kwa wakati ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya elimu na maji inayoendelea kutekelezwa kwenye maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Songea.

Ametoa rai kwa wananchi kuacha tabia ya kuhujumu miundombinu ya umeme ambapo limeibuka wimbi kubwa la wizi wa kebo kwenye transifoma na kusababisha hasara kwa Serikali na amelitaka jeshi la polisi kuhakikisha wanachukua hatua kali kwa yeyote atakayebainika anahusika na matukio hayo.’Alisisitiza’

Amewataka viongozi na wataalamu wa mazingira kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na namna ya kutunza mazingira ikiwemo na utunzaji wa vyanzo vya maji pamoja na misitu katika maeneo yao ili kuthibiti mabadiliko ya tabia ya nchi yaliyosababisha ongezeko kubwa la joto katika maeneo mbalimbali nchini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakurugenzi wa Halmashauri zote 3 zilizopo ndani ya Wilaya ya Songea wameahidi kusimamia kikamilifu utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao pamoja na zoezi zima la utoaji wa mikopo kwa vijana, wanawake na watu wenye mahitaji maalumu kwa kuhakikisha mikopo hiyo inaleta tija na maendeleo kwa vikundi hivyo pamoja na kurejeshwa kwa wakati.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Nelly Duwe ametoa pongezi kwa viongozi wa Wilaya ya Songea kwa kukubali kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama ilivyoainishwa katika Ilani ya chama cha mapinduzi na amewataka kuwashirikisha changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika kipindi cha utekelezaji wa miradi  ili waweze kuzitatua kwa pamoja.

Mwisho.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa