• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MRADI wa ujenzi wa lami nzito Manispaa ya Songea uliogharimu sh.bilioni 13 wafikia asilimia 90

Tarehe ya kuwekwa: October 1st, 2019

MANISPAA ya Songea ni miongoni wa Halmashauri 18 Tanzania zinazotekeleza miradi ya uendelezaji na uboreshaji wa Miji na Manispaa. (Urban Local Goevernment Strengthening Program) 

 Ujenzi wa  barabara hizi  ulianza Julai mosi,2015 na ulitarajiwa kukamilika Juni 30,2016.Mradi huu umetekelezwa na Wakandarasi  wawili, ambapo mara ya kwanza ujenzi ulifanywa na Mkandarasi M/S Lukolo Company  LTD aliyeingia mkataba na Halmashauri wa kujenga KM 8.6 za barabara kwa kiwango cha lami nzito kwa gharama ya  shilingi 14,320,586,464.39 ikijumlishwa na VAT.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Tina Sekambo amesema gharama hiyo ya mkataba  ilifanyiwa mapitio(revised contract ) na kufikia Tshs 11,933,899,897.09 ikijumlishwa na VAT. 

“Muda wa Mkataba ulikuwa ni miezi 24, ambapo  mkataba ulivunjwa tarehe 09/10/2017 baada  ya Mkandarasi kushindwa kukamilisha kazi kwa wakati kulingana na mkataba’’,amesema Sekambo.

Hata hivyo amesema Mpaka Mkataba unavunjwa Mkandarasi alikuwa amelipwa jumla ya Tshs 4,352,975,711.70 kati ya fedha hizo  malipo halisi  ya Mkandarasi yalikuwa Tshs 2,204,887,742.04 na  malipo ya awali (advance payment) yalikuwa Tshs 2,148,087,969.66 .

Amesema kati ya fedha hizo za malipo ya awali, Mkandarasi alikuwa anadaiwa Tshs 1,597,006,612.99, fedha hizo zote zimerudishwa na Bank of Africa tarehe 14/12/2018. Hadi mkataba unavunjwa kazi ilikuwa zimefikia hatua mbalimbali. 

Kulingana na Sekambo,ujenzi wa barabara mara ya pili, ulianza Machi 25,2018 baada ya kazi kutangazwa upya na kumpata Mkandarasi CHINA SICHUAN INTERNATIONAL CORPORATION (SIETCO) ambaye alitarajiwa kukamilisha mradi Septemba 30,2019 ambapo Mhandisi  Mshauri wa mradi huu ni  HOWARD HUMHFREYS (T) LTD.  

“Ujenzi huu unahusisha  barabara za  FFU –Matogoro    -   KM.3.2,Songea girls – Mateka  KM 1.5,Bombambili  – Mwembechai   KM 2.5,Majengo Mitumbani – Yapenda Annex.   KM 1.0,Stendi ya Mlilayoyo -  Polisi Station.  KM 0.4,Matomondo   - planet bar. KM. 0.8 na  Buhemba Annex  - Kalembo   KM 0.9’’,amesema.

Kazi zinazofanyika katika  ujenzi wa barabara ni,Kujenga barabara katika kiwango cha lami nzito zenye urefu wa KM 10.3 na upana wa Mita 8,Kujenga mifereji,Kujenga njia za watembea kwa miguu, Kuweka taa za barabarani,Kujenga Maabara kwa ajili ya kupima sampuli za udongo, Zege na baadhi ya sampuli za lami,(Material Test)

 

 Mradi  huu mpaka kukamilika utagharimu jumla ya Tshs 13,164,965,966 na  gharama ya Mhandisi mshauri  ni Tshs    337,000,000.

Mpaka sasa mradi kwa ujumla umefikia asilimia 90 ya utekelezaji . Mradi huu baada ya kukamilika kwa asilimia 100 utapandisha hadhi ya Manispaa  na  utarahisisha  usafiri na usafirishaji wa mazao, bidhaa na abiria  kutoka katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri  hivyo kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa Manispaa na Wakazi wake.  Pia barabara hizi zitasaidia kupunguza msongamano wa magari na pikipiki katikati ya Manispaa hivyo kupunguza muda wa kuwa barabarani.

Mradi huu unaongeza thamani ya Ardhi  na nyumba zilizopo pembeni mwa barabara.Barabara zinazojengwa zitawekewa taa za barabarani ambazo zitasaidia katika ulinzi na usalama wakati wa usiku hivyo kupunguza matukio ya uhalifu kwa Raia na mali zao. Pia taa zitawasaidia wafanyabiashara wadogo kuongeza muda wa kukufanya  biashara zao wakati wa usiku na hivyo kuongeza  kipato na mzunguko wa fedha ndani ya  Manispaa. 

 Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Septemba 30,2019

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa