• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea amewataka Maafisa Watendaji wa Kata kusimamia usafi wa Mazingira.

Tarehe ya kuwekwa: July 31st, 2024

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea imepongezwa kwa kutozalisha madeni mapya  kutoka kwa wazabuni na wadau mbalimbali ambapo wameitaka Halmashauri hiyo kuendelea kuwa safi bila ya kuwa na  madeni mapya.

Rai hiyo imetolewa kwenye mkutano wa baraza la madiwani uliofanyika tarehe 31 Julai 2024 ambao ulihudhuriwa na Madiwani, Wataalamu, Viongozi wa vyama vya siasa, pamoja na wananchi  uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea ikiwa ni kikao cha baraza la nne kwa mwaka 2023/2024.

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Mheshimiwa Michael Mbano amewataka Maafisa watendaji wa Kata wahakikishe wanasimamia utekelezaji wa zoezi la usafi wa mazingira sambamba na usafishaji maeneo yote ambayo yalilimwa  mahindi wahakikishe  yanaondolewa  sambamba na wananchi kufungua njia/barabara  zilizofungwa ili ziweze kupitika.

Alisema “ Mtakumbuka  mwezi Juni 29 mwaka huu 2024 Halmashauri ya Manispaa ya Songea ilipokea fedha zaidi ya Bil. 4 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo  ambapo kwa mujibu wa maelekezo ya Serikali fedha hizo,  zinatakiwa kutumika kwenye miradi na kuhakikisha  inakamilika ifikapo Septemba 30 mwaka huu, hivyo amewataka wataalamu kunasimamia miradi hiyo  na ikamilike  kwa wakati.” Mhe. Mbano alibainisha.

Amewataka wataalamu kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ambayo yatawezesha kutatua changamoto  za Halmashauri ambapo kwa mwaka 2024/2025 kupitia mapato yake ya ndani ya Halmashauri imetenga bajeti ya kiasi cha Mil 200 kwa ajili ya utengenezaji madawati ya shule, hivyo amewasisitiza  wataalamu hao kuongeza juhudi za ukusanyaji wa mapato hayo.

Aidha amewashauri wataalamu wa Manispaa hiyo kuhakikisha wanashughulikia haraka mchakato wa mabadiliko ya Bendera ya Halmashauri haraka iwezekanavyo  kabla ya kuanza kwa Uchaguzi mdogo wa Serikali za Mitaa ili Bendera hizo ziweze kupeperushwa kwenye kila ofisi ya Serikali za Mitaa.

Akizungumza Katibu Tawala Wilaya ya Songea Ndugu. Mtella Mwampamba amewataka Maafisa maendeleo ya jamii kutumia njia iliyotumika kuelimisha jamii kuweza kukopa mkopo na njia hiyo hiyo itumike kudai madeni hayo ili kuweza kufanikiwa  kukusanya madeni  ya shilingi Bil. 1.3 fedha ambazo ni  marejesho ya vikundi vya Vijana, wanawake na Walemavu ambazo hazijarejreshwa, hivyo amewataka Maafisa Maendeleo ya Jamii kuongeza jitihada za kukusanya fedha hizo ili ziweze kukopeshwa kwenye vikundi vingine vyenye sifa ya kupata mikopo.

 Rai imetolewa  kwenye Baraza hilo kutokana na kubadilika badilika kwa bei ya Mahindi,  hivyo amewataka wananchi kuanzisha utaratibu wa kuuza unga na Pumba za mahindi  badala ya kuuza mahindi pekee ili mkulima aweze kujipatia kipato.

Akizungumza Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Songea Mjini ndugu. James Mgego, ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Songea kwa kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi  pamoja na pongezi hizo,  amewataka  wataalamu kukamilisha miradi Viporo ili iweze kutumika kwa wakati sambamba na kumsemea Mheshimiwa  Dkt. Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa  kazi nzuri anayoifanya pamoja na miradi yote iliyotekelezwa  ili wananchi waweze kufahamu.

Akizunzungumza kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Songea Alto Liwolelu ambapo alisema,  amepokea maagizo yote yalitolewa na viongozi kupitia baraza la madiwani na kuahidi kusimamia ukusanyaji wa madeni ya vikundi  shilingi  Bil. 1.3 fedha zilizotolewa mikopo ya wananwake 4%, Vijana 4% na walemavu 2%,pia  Maafisa watendaji kusimamia safi wa mazingira pamoja na ukuamilishaji wa miradi ya maendeleo. “Alibainisha”

IMEANDALIWA NA;                                                                                                                

AMINA PILLY                                          

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI






Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa