• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA SONGEA AMEWATAKA WAHESHIMIWA MADIWANI KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI SENSA.

Tarehe ya kuwekwa: August 26th, 2022

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea  Michael Mbano amewataka Waheshimiwa Madiwani  na Wataalamu wote kuendelea  kufanya uhamasishaji katika kata zao na kuendelea kuwahimiza wananchi  kujitokeza kuhesabiwa Sensa ya watu na makazi ambayo leo hii ni siku ya nne toka zoezi hilo lianze kufanyika.  

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 26 Agosti 2022 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani  uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kuhudhuriwa na Madiwani, Wananchi mbalimbali, Wataalamu na viongozi wa vyama vya siasa ambacho ni kikao cha kuhitimisha taarifa  kwa mwaka wa  fedha 2021 hadi 2022.

Mbano akihitimisha baraza hilo huku akitoa taarifa za kuwakaribisha wananchi wote katika  Mkutano wa Mwaka  wa Baraza la Madiwani ambao unatarajia kufanyika hapo kesho  tarehe 27 Agosti 2022 katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Akihutubia Mkutano wa Baraza la Madiwani Waziri wa Katiba na Sheria DKT. Damas Ndumbaro(MB) alisema “ Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha Tozo na Kodi  ambayo hulipwa  na wananchi kwa ajili ya Maendeleo ya Taifa letu na hatimaye  hurudishwa asilimia kwenye Halmashauri mbalimbali ambazo husaidia jamii kwa maendeleo ya Nchi yetu”  Alisisitiza.

Alisema Kodi  inasaidia Serikali  kupata Maendeleo ambapo kwa Manispaa ya Songea imesaidia kujenga miradi mbalimbali  ya maendeleo ambapo  katika kipindi cha mwaka 2021/2022 Manispaa ya Songea  imewezesha kujenga vituo vya afya vitano 5, ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya ambayo inajengwa katika kata ya Tanga, Ujenzi wa Masoko mawili ya kisasa ya Manzese, pamoja na ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Ruvuma.

Dkt. Ndumbaro (MB) amebainisha kuwa ataendelea kutatua changamoto  zinazowakabili wananchi wa Jimbo la Songea Mjini  kwa lengo la  kusimamia na kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Hamisi Abdallah Ally amewataka wataalamu kusimamia vizuri zoezi la usajili wa wakulima wanaohitaji pembejeo na kuondoa malalamiko mbalimbali ambayo yanaweza kujitokeza.

Mhe. Hamisi amesema Maafisa kilimo  wanatakiwa  kufanya kazi kwa weredi na kuhakikisha wananchi wanapata pembejeo ya Ruzuku kwa wakati na kwakuwa wamepewa vyombo vya usafiri watatakiwa kuwafikia wakulima kwa wakati na kutatua changamoto zao.

Waheshimiwa Madiwani kwa umoja wao wamepokea maagizo yaliyotolewa kwenye kikao hicho na wameahidi kutoa ushirkiano  kwenye kata zao.

Imeandaliwa na;

AMINA PILLY

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

 

 

 


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa