• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWANAFUNZI HAMZA MASOUD NGOSE NI KINARA WA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA KITAIFA 2022

Tarehe ya kuwekwa: July 19th, 2022

Na;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI 

MANISPAA YA SONGEA.

17.Julai.2022

Mkuu wa Wilaya ya Songea  Pololet  Kamando Mgema ameongoza tafrija  fupi ya kumpongeza Hamza Masoud Ngose mwanafunzi aliyehitimu masomo yake ya kidato cha sita kwa mwaka 2022 katika  Sekondari ya Wavulana Songea, na  kuongoza ufaulu  katika masomo ya sanaa na kupata Daraja la kwanza 1.3 na hatimaye kuibuka kuwa mshindi  wa kwanza  kitaifa.

Tafrija  hiyo imefanyika hapo 15 Julai 2022 katika shule ya Sekondari ya Wavulana Songea iliyopo kata ya Seedfarm Manispaa ya Songea Mkoa  wa Ruvuma, iliyohudhuriwa  na viongozi mbalimbali ngazi ya Mkoa, Wilaya, Halmashauri, Wanafunzi, na wadau mbalimbali.

Pololet  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambapo alisema “Miongoni mwa vijana waliokutana  na changamoto  ya kukosa  haki ya kusoma  kutokana  na sababu  ya ulemavu wa kutoona ni Hamza Masoud Ngose,  baada ya kutokea changamoto hiyo wazazi wa mwanafunzi huyo walifanya jitihada za kutafuta  shule inayoendana na mazingira na  alihitimu masomo ya msingi  na kujiunga masomo ya Sekondari katika shule ya Sekondari ya Wavulana Songea.” 

Aliongeza kuwa baada ya  kuhitimu masomo ya kidato cha nne  alifaulu  na kupata  daraja la kwanza 1.9 ambapo kwa mwaka 2022 mwezi Mei alihitimu masomo yake ya kidato cha sita ambapo alifaulu na kupata daraja 1.3 kwanza na kuwa wakwanza Kitaifa katika masomo yake  ya Sanaa. “Alimpongeza .“

Alisema kutokana na ufaulu wa masomo yote daraja A imewezesha kupanda kwa ufaulu wa shule na kuwa nafasi ya 16 kati ya shule 27 za Sekondari za kidato cha sita Mkoani Ruvuma, nafasi ya  264 kati ya 644 katika shule  ambazo zina kidato cha sita.

Halmshauri ya Manispaa ya Songea  imemzawadia Hamza Masoud Ngose  kiasi  cha shilingi 1,000,000, zawadi ya Jina la bweni ambalo litaitwa Hamza  Masoud Ngose  ambalo linatarajia kujengwa pamoja na zawadi mbalimbali  kutoka kwa  Mkuu wa Wilaya ya Songea, na  Chama cha Walimu (CWT).

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho  alisema kuwa Serikali  ya awamu ya sita inathamini  sekta ya Elimu kwa kufanya maboresho ya miundombinu mbalimbali ya elimu ili kuwezesha kuinua kiwango bora cha elimu nchini.

Oddo, ametoa wito kwa wanafunzi wote Mkoani Ruvuma kusoma kwa bidii kama mwanafunzi Hamza Masoud Ngose ambaye ameonesha jitihada za dhati katika kipindi cha masomo na hatimaye kufaulu mtihani wa kidato cha sita na kuongoza kuwa mwanafunzi wa kwanza kitaifa.” Oddo, Alimpongeza.”

Naye Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano amewapongeza  walimu pamoja na wanafunzi kwa jitihada walizozifanya katika kufanikisha  ufaulu wa mtihani wa kidato cha sita uliofanyika mwezi mei 2022 ambapo mwanafunzi Hamza Ngose amefanya vizuri na kuongoza kitaifa ambapo alisema kupata ulemavu haimaanishi ukate tamaa ya maisha.

Naye Mkuu wa shule ya Sekondari ya wavulana Songea Gelalus Gerion Lugome alibainsha kuwa takwimu za maendeleo  ya kitaaluma za mwanafunzi zimekuwa zikijipambanua zenyewe  kwa ubora wake ambapo kwa mwaka 2019 akiwa kidato cha nne alipata daraja la kwanza akiwa na alama  ‘A’sita  katika masomo 7  huku akiwa amepata  taalma  C  katika somo kwa njia ya vitendo likiaminika kuathiri ufaulu wake.

Luogome alielleza kuwa, Hamza Masoud Ngose alijiunga na kidato cha tano mwaka 2020 katika kipindi cha masomo yake aliwahi kugombea na kupata ushindi wa kishindo nafasi ya mwenyekiti wa Serikali ya wanafunzi na aliongoza bila pasipo kuathiri malengo ya kitaalma.

Naye mwanafunzi Hamza Masoud Ngose ametoa shukrani kwa uongozi ngazi ya Mkoa, Halmashauri na walimu pamoja na Serikali ya awamu ya sita  kwa kuboresha elimu nchini ambayo imepelekea kufanya vizuri katika mitihani na kupelekea kufaulu kuwa mshindi wa kwanza kitaifa katika masomo ya Sanaa. “Aliwashukuru.”

Aliongeza kuwa kupitia tafrija iliyoandaliwa dhidi yake itamsaidia  kufungua fursa za yeye kwenda kusoma elimu ya juu, huku  akiiomba  Serikali imsaidie kumsomesha ili aweze kutimiza ndoto yake.

Aidha kwa upande  wazazi wa Hamza Masoud Ngose  wameishukuru Serikali  kwa matokeo mazuri ya mtoto wao, pamoja na tafrija fupi iliyoandaliwa na Serikali kwa ajili ya kumpongeza mtoto wao pamoja na zawadi zilizotolewa.    “ Walishukuru” 

Mwisho.


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa