• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru kukimbizwa kesho Manispaa ya Songea

Tarehe ya kuwekwa: June 6th, 2018

Manispaa ya Songea mwaka huu imedhamiria kuibuka kidedea katika mashindano ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru baada ya kuweka maandalizi mazuri.

Mwenge wa Uhuru Manispaa ya Songea unatarajia kupokelewa kesho Juni 7,2018,katika shule ya Msingi Mang’ua Kata ya Lilambo na unatarajiwa  kukabidhiwa katika Halmashauri ya Madaba Juni 8 mwaka huu.

Kwa mujibu wa Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Manispaa ya Songea Faraja Yonasi,Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Manispaa ya Songea unatarajia kutembelea,kuweka mawe ya Msingi na kuzindua miradi mbalimbali.

Kulingana na Ratiba ya Mwenge jumla ya miradi tisa yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 945 inatarajiwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru. Miongoni mwa miradi hiyo ni mradi wa zahanati binafsi ya St Benjamin iliyopo katika Kata ya Msamala. Mwenge wa Uhuru unatarajia kufanya uzinduzi wa zahanati hiyo.

Miradi mingine ambayo inatarajiwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru ni mradi wa mabwawa ya kisasa ya ufugaji samaki na utalii wa ndani Luhira kata ya Msamala, mradi wa maji Mitendewawa kata ya Mshangano, mradi wa madarasa matatu shule ya msingi Kibulang,oma kata ya Lizaboni, mradi wa kopa ng,ombe lipa ng'ombe kata ya Lilambo, mradi wa kiwanda cha kukoboa mpunga katika Kata ya misufini na mradi wa ofisi ya Kata ya Mjimwema.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema ameendelea  kuwasisitizia wakuu wa Idara,Vitengo,madiwani na maafisa watendaji kushirikiana kujenga hamasa ili kuhakikisha kuwa Manispaa hiyo mwaka huu inashika nafasi za juu kwenye mashindano ya Mbio za Mwenge wa Uhuru.

“Haya ni mashindano,vimewekwa vigezo ili kushinda,sitaki mchezo katika suala la Mwenge,atakayeshindwa kuwajibika,tutachukuliana hatua,Mwenge ni sherehe ili kufanikiwa kila mmoja ni lazima atekeleze majukumu yake’’,anasisitiza Mkuu wa Wilaya.

Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018;

-Elimu ni Ufunguo wa maisha

-Wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu

-Mwananchi jitambue pima afya yako

-Kataa rushwa jenga Tanzania

-Shiriki kutokomeza malaria

-Tuwasikilize na kuwashauri watoto wasitumie dawa za kulevya

Taarifa imetolewa na

Albano Midelo

Afisa Habari na Mawasiliano,Manispaa ya Songea

Juni 6,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa