• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru watembelea na kukagua mradi wa stendi mpya ya mabasi Songea

Tarehe ya kuwekwa: September 26th, 2019

Manispaa ya Songea ni miongoni mwa Halmashauri 18 Tanzania zinazotekeleza miradi ya uendelezaji na uboreshaji wa Miji na Manispaa. (Urban Local Goevernment Strengthening Program).

Ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi unafanyika katika eneo lenye ukubwa wa hekari 15 lilipo katika Kata ya Tanga kilomita 12 toka katikati ya Manispaa ya  Songea.  Ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi Songea, ulianza tarehe 25/03/2018 na unatarajiwa kukamilika tarehe 30/09/2019. Ujenzi unafanywa na Mkandarasi CHINA SICHUAN INTERNATIONAL CORPORATION (SIETCO) na kusimamiwa na Mhandisi  Mshauri  BUREAU FOR INDUSTRIAL CORPORATION (BICO) ambao ni Chuo kikuu cha Dar –es- salaam. Ujenzi huu unahusisha kazi zifuatazo:-

  1. Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami nzito zinazoingia, kutoka na kuzunguka  kituo cha mabasi zenye urefu wa kilomita 2.  Upana wa  barabara zinazoingia na kutoka ni mita  7 na barabara zinazozunguka  kituo cha mabasi  ni mita 12.
  2. Ujenzi wa mifereji ya barabara.
  3. Ujenzi wa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 17,100 la kuegesha mabasi lenye uwezo wa kuegesha mabasi 92 kwa  wakati mmoja. Vilevile kutakuwa na vibanda vya abiria kusubiria mabasi (shadee) 48.
  4. Ujenzi wa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 1800 la kuegesha Taxi lenye uwezo wa kuegesha Taxi 60 kwa wakati mmoja
  5. Ujenzi wa maduka 30
  6. Ujenzi wa ofisi za kukatia tiketi 20
  7. Ujenzi jengo la Utawala
  8. Ujenzi wa vyoo

10.Ujenzi wa jengo litakalokuwa na Kituo cha Polisi na Ofisi za uhamiaji

11.Ujenzi wa kisima cha maji safi chenye urefu wa mita 75

12. Kuweka mfumo wa maji  safi  na maji taka

13. kuingiza umeme wa TANESCO

14. Kuweka  Taa za sola

, Mradi huu mpaka kukamilika utagharimu jumla ya Tshs 6,189,340,930.Mpaka sasa Mkandarasi amelipwa kiasi cha Tshs 4,112,445,048.53 ikiwa ni pamoja na malipo ya awali (Advance payment).  Gharama za Mhandisi  mshauri ni 319,571,801.60 kati ya  fedha  hizo amelipwa Tshs 180,748,637.51. Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 88.

Ujenzi wa kituo kikuu cha Mabasi, umetoa ajira kwa Wananchi 250 Kati ya hao Wataalam ni 41 na wanaobaki ni Wasaidizi mbalimbali waishio katika Kata ya Tanga na Manispaa  kwa ujumla hivyo kuongeza kipato kwa Wananchi.  Aidha Mradi huu baada ya kukamilika utaisaidia Halmashauri  kuongeza  bajeti  ya mapato  ya ndani  ya mwaka  2020/2021 toka Tshs 3,749,258,100.00 mpaka Tshs 3,958,478,100.00 sawa na ongezeko la asilimia  5.29.  Pia unatarajiwa kutoa ajira kwa Wananchi 396 kwa mchanganuo ufuatao:-  madereva na wafanyakazi wa mabasi 306, Wauza maduka 30 Wakatisha Tiketi 60 na Wafanyabiashara ndogondogo wakiwemo mama lishe na Wamachinga.

 Mradi huu baada ya kukamilika utaboresha utoaji wa huduma na  utaimarisha usalama wa abiria kutokana na kuwepo kwa kituo cha Polisi na  Ofisi za uhamiaji ndani ya kituo cha Mabasi.

Imetolewa na Kitengo cha Habari Manispaa ya Songea

Septemba 26,2019


Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa