• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENYEKITI CCM WILAYA YA SONGEA AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MANISPAA YA SONGEA.

Tarehe ya kuwekwa: June 16th, 2020

Kamati ya siasa ccm Wilaya ya Songea imefanya ziara ya kukagua baadhi ya miradi mbalimbali ambayo imetekelezwa na serikali ya awamu ya tano ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha mapinduzi (CCM) inayoongozwa na Mh. Rais John Pombe Magufuli, iliyofanyika tarehe 10-11/06/2020 manispaa ya Songea.

Ziara hiyo iliyoongozwa na M/kiti wa CCM Wilaya ya Songea  Hamisi Abdallah Ally akiwa  pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Siasa Wilayani humo ambapo waliweza kutembelea baadhi ya Miradi iliyopo Manispaa ya Songea na Kushuhudia utendaji kazi na usimamizi Bora wa miradi iliyojengwa kwa nguvu za Wananchi na  Serikali.

Miongoni mwa Miradi iliyokaguliwa na kamati hiyo ya Siasa ni pamoja na;                          Ujenzi wa Zahanati  ya Likuyufusi ambayo ipo hatua ya kuezekwa, Mradi wa upimaji Viwanja vidogovidogo kata ya Lilambo, Mradi wa Maji Lilambo A na Lilambo B ambao umesanifiwa kuhudumia wakazi wapatao  11,981 kwa Gharama Zaidi ya  Tsh Bil 1 ambazo Zimetumika na mradi umeshakamilika, Ujenzi wa zahanati Kata ya Ruhuwiko ambao upo hatua ya ukamilishaji, Mradi wa ujenzi wa kiwango cha lami wa njia ya kuruka na kutua ndege yenye urefu wa mita 1,740 na upana  mita 30 ambao uanendelea kujengwa, Ujenzi wa Zahanati ya Makambi  Kata ya Ndilimalitembo ambayo ipo hatua ya ukamilishaji, ujenzi wa Barabara ya  Tunduru JCT- Seedfarm km 0.75 kwa kiwango cha Lami nyepesi (double surface Dressing) ambao umegharimu bil 33.4 hadi kukamilika,  Ujenzi wa daraja la Fataki kwenye  barabara ya Songea- Namtumbo ambao bado haujakamilika,  Mradi wa Usambazaji wa Umeme wa “REA” Ruhila Seko ( hot line 1.2 km),  Kukagua mradi  jengo la Maabara na choo Sekondari ya Subira,  kuwatembelea Wanufaika wa mradi wa TASSAF Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani,  pamoja na kukagua  vikundi vya wanawake, vijana, na walemavu vilivyowezeshwa kupata mkopo  kutoka kwa  Mkurugenzi Manispaa kupitia Maendeleo ya Jamii.

Hamisi,  akitoa pongezi kwa  Mkurugenzi  Manispaa ya Songea katika kusimamia vizuri ujenzi wa Miradi hiyo ambayo imefikia hatua nzuri, na  ikiwa   baadhi ya miradi hiyo kuwa  imekamilika na kuanza kutumka, na miradi mingine kunaendelea na ujenzi. Hata hivyo “ alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa kukamilisha miradi hiyo haraka iwezekanavyo ili kusogeza huduma   kwa wananchi  ambao hutembea mwendo mrefu kufuata matibabu. Akitaja baadhi ya Zahanati ambazo zinahitaji ukamilishaji wa haraka ni pamoja na Zahanati ya Lilambo, Ruhuwiko, na Makambi.” Alisisitiza.

IMEANDALIWA NA; 

AMINA PILLY

KAIMU AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa