• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU MEYA MANISPAA ASISITIZA UWAJIBIKAJI WA VIONGOZI KWA JAMII.

Tarehe ya kuwekwa: February 16th, 2021

Ushirikishwaji na uwajibikaji wa viongozi kwa  wananchi ni  sehemu ya utawala bora kwa kiongozi, hivyo kila Mheshimiwa diwani katika Kata yake anatakiwa kuwashirikisha wadau wa maendeleo waliopo kwenye kata husika kwa ajili ya kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.

Hayo yametamkwa na Naibu Meya Jeremia Milembe kwa niaba ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Michael Mbano   katika  kikao  kazi ambacho kilihudhuriwa na  Maafisa watendaji wa kata, Waheshimiwa Madiwani, pamoja na Wakuu wa Idara kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Songea leo 16 februari 2021.

Jeremia alisema katika kikao kijacho atahitaji  uwepo wa  taarifa kutoka kila kata  zikionesha aina ya changamoto na jinsi alivyoweza  kuitatua ili waweze kubaini njia ya kusaidia kuzitatua changamoto zinazowakabili wananchi wa kata husika.

Kikao hicho  hufanyika kabla ya kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ambacho hufanyika kwa  lengo la  kupokea taarifa mbalimbali za utekelezaji kutoka kila kata zinazojumuisha maendeleo ya elimu, miundombinu ya shule, Zahanati, maendeleo ya kilimo, mifugo, hali ya majanga, utawala, Uchumi, uimarishaji wa dhana ya uzalendo pamoja na kupokea changamoto mbalimbali kutoka kwenye kata na kufanyiwa ufumbuzi.

Jeremia amewataka wataalamu wa Manispaa kutoa ushirikiano kwa Madiwani ili kujenga ufanisi wa kiutendaji katika kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kwa lengo la kutoa huduma bora kwa jamii ya Songea.

Naye  Afisa utumishi Mkuu Manispaa ya Songea Lewis Mnyambwa akitoa ufafanuzi kuhusu kikao cha utekelezaji ambapo  alisema  “ kanuni za kudumu za Halmashauri ya manispaa ya Songea Tangazo la Serikali Na 162 inasema taarifa za utekelezaji kutoka katika kata zitawasilishwa na Diwani wa kata husika au kama diwani hayupo, taarifa hiyo itawasilishwa na Diwani wa Viti maalum anayeishi katika Kata hiyo na kama Diwani Viti Maalum hayupo, Meya atamtaarifu mapema Diwani yeyote ili ajiandae kuwasilisha taarifa hiyo”.

Baraza hilo la Madiwani linatarajia kufanyika kesho 17.02.2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea kuanzia muda wa  saa tatu asubuhi.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

16 .02.2021



Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa