• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI DKT.ANGELINE MABULA ATOA AGIZO KWA WADAIWA SUGU WA KODI YA ARDHI.

Tarehe ya kuwekwa: February 25th, 2021

ENDAPO ulipewa Ilani ya siku 14 inayokutaka kulipa kodi ya ardhi na haijalipwa kodi hiyo  utatakiwa kupelekwa kwenye baraza la ardhi na endapo hatalipa kodi hiyo atauziwa mali zake.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi DkT.Angeline S.L.Mabula akiwa  ziarani Manispaa ya Songea iliyofanyika tarehe 24 februari 2021 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea na kugawa hati 64 za umiliki wa ardhi.

DKT. Mabula alisema Lengo kuu la Serikali ni kumuongoza mwananchi wa kawaida katika kupata Hati yake ya umiliki wa ardhi ili awe anauwezo wa kutambua mipaka yake,  kutatua migogoro, pamoja na kutumia  kukopa fedha Benki sababu Hati ni pesa.

Alisema Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali  umekuwa chini sana ukilinganisha na hali halisi ya makusanyo ya maduhuli ambapo  hadi hivi sasa makusanyo hayo yamefikia 16%  kimkoa  ambayo hadi  kufikia june hatarajii kama watafikia 50%.

Alieleza kuwa sheria ipo wazi hata mwenye kiwanja ambacho hakina HATI anatakiwa kulipa kodi ya ardhi ambapo alisema kifungu cha 48 kifungu kidogo cha (1) G cha sheria namba (4) ya ardhi kinasema “unapopewa  Ilani na ukakaanayo bila kulipa ndani ya miezi 6 ubatilishwaji wa umiliki unaweza kufanyika bila kupewa taarifa kwasababu tayari umekiuka sheria.”

Aliongeza kuwa kifungu cha 33 cha sheria namba (4) ya mwaka 1999 kwa marekebisho yaliyofanyika kwenye sheria ya fedha mwaka 2020 ambayo inasema “ yeyote mwenye kumiliki ardhi bila kujali ana HATI au hana HATI anatakiwa kuomba kumilikishwa ardhi na endapo hajaomba kumilikshwa atatakiwa kulipa kodi toka pale ambapo idhini ya ramani zake zilipitishwa.”

Ameagiza kutokana na wadaiwa sugu kuwa wengi na wengine kesi zao zipo kwenye mabaraza na wengine wana order na zimeshapelekwa kwenye baraza za ardhi ambapo amesema utekelezaji wake uanze sasa kwa kukamata mali zao na kuziuza ili kodi iweze kukusanywa kwa kiasi kikubwa.

Agizo hilo linatakiwa kutekelezwa mara moja na hadi kufikia aprili 31 utekelezaji wa sheria ambazo zilikuwa hazitekelezwi uwe umeanza kutekelezwa. Alisema DKT. Mabula.

Naye Kamishina wa ardhi Msaidizi Mkoa wa Ruvuma Ildefonce Ndemela alisema tangu kuanzishwa kwa ofisi ya Ardhi Mkoa, Ofisi imesimamia  na kutekeleza kazi za upangaji, upimaji, umilikishaji, uthamini,usajili wa Hati na nyaraka mbalimbali, utatuzi wa migogoro ya Ardhi na ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kama utawala wa Ardhi ambapo katika mwaka wa fedha 2019/2020 Mkoa wa Ruvuma ulipangiwa kukusanya fedha 1,076,957,356.22 sawa na 108%, ambapo kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Mkoa wa Ruvuma umepangiwa lengo la kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 4.6.

IMEANDALIWA NA;

AMINA PILLY;

AFISA HABARI MANISPAA YA SONGEA.

25.02.2021

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa