• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU Waziri wa Elimu aagiza VETA Songea kufundisha kozi za utalii na zana za kilimo

Tarehe ya kuwekwa: October 1st, 2018

Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ametoa wiki moja kwa mtaalamu Elekezi kutoka Kampuni ya Archquants Service Limited kuhakikisha inawasilisha michoro ya kazi za nje ya Chuo cha ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Namtumbo kilichoko Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma ili chuo hicho kiweze kukamilika na kuanza kazi.

Naibu Waziri Ole Nasha ametoa agizo hilo Mkoani Ruvuma wakati wa kukagua maendeleo ya ujenzi wa chuo hicho ambapo amesema ucheleweshwaji wa michoro hiyo unapelekea kuchelewesha ukamilishaji wa mradi huo.

Awali Mkandarasi anayejenga Chuo hicho CF Builders alimweleza Naibu Waziri kuwa mpaka sasa hajapokea michoro ya kazi za nje ya Chuo hicho jambo ambalo linasababisha kuchelewa kukamilisha mradi huo.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Ole Nasha ameitaka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA kuhakikisha   wanaanzisha kozi ya ufundi wa zana za kilimo (agro mechanics) katika Chuo cha Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi cha Songea VETA ili kuweza kupata vijana wengi watakaoweza kusoma kozi hiyo.

Alisema ukanda wa Nyanda za Juu Kusini unategemea sana kilimo na asilimia 60 ya chakula hutoka huko katika ukanda huo hivyo kuanzisha kozi hiyo itasaidia wananchi wengi kuweza kupata uelewa wa kile wanachokisoma katika kukifanyia kazi.

Alisema Nchi yetu iko kwenye jitihada za kufikia uchumi kati ambao unategemea msukumo wa viwanda na kama unazungumzia masuala ya uchumi wa viwanda ni lazima kuwa na mafundi hivyo Vyuo vya VETA vitasaidia kupata nguvu kazi watakaosaidia katika uchumi wa viwanda.

“Serikali inatilia mkazo Elimu ya ufundi  na imejielekeza katika kuhakikisha inapanua fursa ya vijana wengi kupata hiyo na ndio maana unaona  Serikali ya awamu ya tano imeamua kuweka Vyuo vya VETA katika kila Wilaya na Mkoa” Alisisitiza Naibu Waziri Ole Nasha

Ameipongeza VETA Songea kwa namna ambavyo wamebuni mbinu mbalimbali za kufikisha Elimu ya ufundi kwa wananchi wengi kwa kuwafikia katika maeneo yao na kuwataka kuendelea kushirikana na makampuni na mbalimbali wanapotoa mafunzo yao ili kujua uhitaji wa soko.

Naibu Waziri Ole Nasha yuko mkoani Ruvuma kwa siku mbili kukagua miradi ya Elimu inayotekelezwa na Wizara katika Wilaya za Namtumbo na Songea.

Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

01/10/2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa