• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NFRA Kanda ya Songea kununua mahindi tani 7000

Tarehe ya kuwekwa: July 19th, 2018

WAKALA wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula(NFRA) Kanda ya Songea imependekeza kununua mahindi ya akiba ya serikali tani 7000 katika kipindi cha kuanzia Julai 2018 hadi Juni 30,2019.

Mkoa wa Ruvuma katika kipindi cha mwaka 2017/2018 umezalisha mahindi tani 933,284.Akitoa taarifa ya NFRA kwa niaba ya Meneja wa Kanda ya Songea Eva Kwavava katika kikao kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga,amesema mgawo wa tani hizo unazingatia taarifa za uzalishaji wa kila Halmashauri.

Kikao hicho ambacho kimefanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea kimewashirikisha,wabunge wa mkoa wa Ruvuma, wakurugenzi,wenyeviti wa Halmashauri, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea,wakuu wa wilaya, makatibu tawala wa wilaya na watalaam wa kilimo na ushirika.

Viongozi hao kwa pamoja wameridhia mapendekezo hayo na kushauri kutafuta fedha ya kuongeza ununuzi wa mazao kwa sababu tani zilizopendekezwa kununuliwa na serikali ni kidogo ukilinganisha na uzalishaji.

Hata hivyo Kaimu Meneja huyo wa NFRA amesema bei elekezi ya ununuzi wa mahindi na tarehe ya kuanza kununua itatajwa wakati wowote kuanzia sasa baada ya mchakato kukamilika.

Mapendekezo ya malengo ya ununuzi kwa mwaka 2018/2019 katika mkoa wa Ruvuma yanaonesha kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mgawo ni tani 417 wakati kiasi kilichozalishwa ni tani 58,144,Halmashauri ya Wilaya ya Songea tani 1,983.531,kiasi kilichozalishwa ni tani 227,320 na Halmashauri ya Madaba tani 1,216.466 na kiasi cha tani zilizozalishwa ni 148,408.

Kulingana na mapendekezo hayo Halmashauri ya wilaya ya Mbinga imepangiwa kununua tani 1,189.175,kiasi kilichozalishwa ni tani 165,484,Halmashauri ya Mbinga Mji tani 461.976 na kiasi cha tani zilizozalishwa ni 64,288.

Katika Wilaya ya Namtumbo zitanunuliwa tani 1,068.017,kiasi kilichozalishwa ni tani 134,708,Nyasa tani 663.011 na kiasi kilichozalishwa ni tani 64,432 na wilaya ya Tunduru imezalisha tani 70,500 za mahindi na hakuna wa ununuzi.

Katika msimu wa mwaka 2017/2018 Kanda ya Songea ilipangiwa kununua mahindi tani 6,182,hata hivyo kanda hiyo ilinunua jumla ya tani 11,557,529 baada ya malengo kuongezwa mara mbili.

Kaimu Meneja wa NFRA Kanda ya Songea amesema katika kituo hicho kilichopo Ruhuwiko mjini Songea,kuna tani 21,892.924 za mahindi ambayo yanatokana na ununuzi wa misimu miwili ya 2016/2017 na 2017/2018 na kwamba akiba hiyo ipo katika hali nzuri.

Pamoja na kupitisha mapendekezo hayo wajumbe wa kikao hicho wameshauri kipaumbele cha ununuzi kiwe kwa wakulima wadogo badala ya wakulima wafanyabiashara na njia za ununuzi ziwe katika vyama vya ushirika na ununuzi kupitia vituo vya ununuzi vitakavyopangwa katika kila Halmashauri.

Wajumbe hao pia wameshauri mipaka ya nchi isifungwe ili kuruhusu soko la mahindi nje ya nchi,kusimamia ubora za mahindi,kutoa elimu na kuhamasisha wananchi wajitokeze kwenye vituo vya kununulia mazao mara vitakapotangazwa.

Imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Julai 19,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa