• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NGONO zembe inavyoongeza kasi ya maambukizi mapya ya HIV Songea

Tarehe ya kuwekwa: May 10th, 2018

KASI ya maambukizo mapya ya virusi vya UKIMWI katika Kata ya Ruhuwiko Manipaa ya Songea mkoani Ruvuma inatishia ustawi wa jamii baada ya kata hiyo kuwa miongoni mwa Kata 10 zenye maambukizi ya kutisha kati ya kata 21 zilizopo Manispaa ya Songea.

Taarifa ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI iliyotolewa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani,inaonesha kuwa hali ni mbaya ambapo hivi sasa hadi watoto wadogo wapo katika hatari ya kupata maambukizi.

Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani Kata ya Ruhuwiko Angelina Haule anaelezea namna watoto wa awali walivyo katika hatari ya kupata maambukizi ambapo ameshuhudia katika Mtaa wa Ruhuwiko Kanisani Baadhi ya watu wametumia mpira ya kujikinga na virusi vya UKIMWI yaani kondom na kuitupa hovyo ikiwa na uchafu ambapo watoto wadogo wameonekana baadhi ya maeneo wakipuliza mipira hiyo hali ambayo inahatarisha afya za watoto hao wasiokuwa na hatia.

"Mimi mwenyewe nimewakuta watoto wanaosoma darasa la awali wakipuliza kondom ambazo zimetumika kwa kweli inasikitisha sana ndugu zangu'',anasisitiza Haule wakati anazungumza na wananchi wake.

Mratibu Kinga(CHAC) katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea Zale Makaburi anazitaja Kata ambazo maambukizi ya virusi vya UKIMWI yapo juu kuwa ni Mateka, Bombambili, Mshangano, Lizabon,Lilambo na Ruhuwiko.

Takwimu zinaonesha kuwa watu 10,097 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea  wanaugua UKIMWI na wapo kwenye dawa hadi sasa ambapo Zaidi ya watu 21,000 katika Manispaa hiyo wanaishi na virusi vya UKIMWI.

Taarifa ya kamati Shirikishi ya kudhibiti UKIMWI iliyotolewa kwenye mkutano wa mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea,inaonesha kuwa kiwango cha maambukizi katika Manispaa hiyo kimepungua toka asilimia 4.2 hadi kufikia asilimia 3.7.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Halmashauri ya Manispaa ya Songea ina jumla ya vituo 24 vinavyotoa huduma za Tiba na matunzo kwa waathirika wa ugonjwa wa UKIMWI.

Mratibu wa UKIMWI na tiba katika Manispaa ya Songea Dk.Felista Kibena ameyataja makundi ambayo yanaongoza kwa maambukizi mapya ya UKIMWI kuwa ni watu wanaofanya biashara ya ngono,wanaofanya ngono  ya jinsia moja,wanaojidunga sindano na pamoja na wabwia unga na dawa za kulevya.

Kibena amesema idara yake imeamua kutoa elimu ya ukweli kuhusu UKIMWI katika makundi hayo baada ya utafiti kubaini makundi hayo sasa yanaongoza kwa kiwango kikubwa cha maambuzi ambacho ni asilimia 36 sawa na kila watu 100,watu 36 wana virusi vya UKIMWI.

Hata hivyo amesema kiwango cha maambukizo cha watu wa kawaida ni asilimia tano sawa na kila watu 100,watu watano wana virusi vya UKIMWI.

Mkoa wa Ruvuma unashika nafasi ya tano kitaifa ukiwa na maambukizi ya asilimia saba ambapo mkoa wa Njombe ndiyo unaongoza kitaifa ukiwa na asilimia  14.5,nafasi ya pili inashika na Mkoa wa Iringa,ikifuatiwa na Mkoa wa Mbeya kwa nafasi ya tatu na Mkoa wa Rukwa ukiwa nafasi ya tano.

Taarifa imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Manispaa ya Songea

Mei 10,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa