• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NGURUWE 864 wateketea kwa homa ya nguruwe Songea

Tarehe ya kuwekwa: March 25th, 2018

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Tina Sekambo amesitisha uchinjaji wa nguruwe katika maeneo yote ya Manispaa hiyo tangu Februari mwaka huu, kufuatia kuibuka kwa homa ya nguruwe ambayo haina kinga wala tiba.

Takwimu ambazo zimetolewa na Afisa Mifugo na Uvuvi wa Manispaa ya Songea,Bilaly Mwegeni zinaonesha kuwa homa ya nguruwe(African Swine Fever) katika kipindi cha kuanzia Januari 31,2018 hadi Machi 14,2018 imeua nguruwe 864.

Hata hivyo amesema takwimu hizo za vifo ni matukio ambayo yameripotiwa katika Idara yake ambapo uchunguzi umebaini kuwa zaidi ya nusu ya nguruwe walipo Songea wamekufa kutokana na ugonjwa huo, hali ambayo inataharisha kuteketeza nguruwe katika Manispaa hiyo.

“Takwimu zinaonesha kuwa Manispaa ya Songea ina nguruwe 4581,tukifanya sensa ya idadi ya nguruwe waliobakia katika Manispaa yetu,naamini watakuwa hawazidi 2000,kwa sababu kuna nguruwe wengi wamekufa na takwimu za vifo hazijaletwa ofisini kwetu’’,anasisitiza Afisa Mifugo Mwegeni.

Mwegeni anazitaja kata ambazo zinaongoza kwa vifo vya nguruwe kuwa ni NdilimaLitembo vifo (334),Lizaboni (138), Msamala(90), Matarawe(66) na Ruhuwiko(34) na kata nyingine vifo vya nguruwe ni sio zaidi ya nguruwe watano.

Kutokana na kuenea kwa Homa ya Nguruwe (African swine fever) katika Manispaa na ili kuzuia usambaaji zaidi wa Homa ya Nguruwe Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea  aliagiza watendaji wote wa Mitaa na Kata kuanzia sasa wahakikishe hakuna mtu, kuchinja nguruwe, kusafirisha nguruwe,kuingiza na kutoka katika maeneo ya Manispaa.

Hata hivyo uchunguzi umebaini ugonjwa wa homa ya nguruwe upo katika Halmashauri tatu za Mkoa wa Ruvuma ambazo ni Halmashauri ya Manispaa ya Songea,Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

Kutokana na hali hiyo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma imeitisha mkutano wa wadau wa sekta ndogo ya nguruwe,Machi 26 mwaka huu kukutana kwenye ukumbi wa Maliasili mkoa kwa lengo la kujadili mkakati wa kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo na namna ya kudhibiti ueneaji wake.

Ugonjwa wa homa ya nguruwe hauna kinga.Hata hivyo ugonjwa huo hauna madhara kwa binadamu ambapo kitaalam nguruwe aliyekufa kwa ugonjwa huo anatakiwa kuzikwa katika shimo lililopuliziwa dawa ya kuteketeza virusi lenye urefu wa zaidi ya meta moja.

Taarifa imetolewa na Albano Midelo

Afisa Habari Manispaa ya Songea

Machi 25,2018

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa