• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NMB ilivyofanikiwa kumaliza upungufu wa madawati shule ya msingi Mipeta

Tarehe ya kuwekwa: December 6th, 2018

BENKI ya NMB imefanikiwa kumaliza changamoto ya madawati katika shule ya msingi Mipeta iliyopo katika Kata ya Muhukuru,Halmashauri ya Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Songea Frank Rutakwa  akizungumza katika kijiji hicho kabla ya kukabidhi msaada wa madawati 150 yenye thamani ya shilingi milioni 10,amesema Benki hiyo imeamua kutoa msaada huo baada ya kupata taarifa kupitia vyombo vya habari kuhusu upungufu wa madawati katika shule hiyo.

Anasema NMB imeamua kushirikiana na shule ya Msingi Mipeta kwa kuchangia madawati imara yenye vyuma na kwamba Benki hiyo imekuwa inapokea maombi mengi ya kuchangia miradi mbalimbali.

Rutakwa amesema changamoto katika sekta ya elimu ni miongoni mwa vipaumbele vya Benki ya NMB kwa kutambua kuwa elimu ni uti wa mgongo wa Taifa lolote hapa duniani.

“Tunatambua juhudi za serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli ya kusimamia elimu kwa nguvu zote na kusaidia kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari’’,anasisitiza Rutakwa.

Anasema mchango wa madawati katika shule hiyo ni kuonesha kwa vitendo ushiriki wa NMB kwa vitendo ili kuhakikisha jamii inayozunguka inafaidika na uwepo wa Benki ya NMB ambayo ipo karibu na jamii.

Amesema kwa miaka kadhaa sasa NMB imekuwa inashiriki katika miradi ya maendeleo kwa kujikita katika sekta ya elimu na afya na kusaidia majanga yanapotokea katika maeneo mbalimbali nchini.

Kulingana na Kaimu Meneja huyo wa Kanda,katika kipindi cha mwaka 2018,NMB imetenga shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya jamii ikiwemo kuchangia sekta ya afya na elimu na kwamba kiasi hicho kinaifanya NMB kuwa Benki ya kwanza kuchangia maendeleo kuliko Benki yeyote nchini.

Akizungumza katika hafla hiyo Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mipeta,Henry Kihwili,amesema shule hiyo kata ya Muhukuru ilianzishwa mwaka 2002 ipo umbali wa kilometa 108 toka mjini Songea na umbali wa kilometa 62 toka makao makuu ya kata.

Kihwili anabainisha zaidi kuwa shule hiyo ina jumla ya wanafunzi 354 wanaosoma kuanzia darasa la Awali hadi la sita na kwamba shule hiyo ina jumla ya walimu sita.

Mkuu huyo wa shule ameipongeza NMB kwa msaada wa madawati 150 ambayo yamemaliza changamoto ya upungufu wa madawati katika shule hiyo.

Kihwili anasema kabla ya msaada wa madawati hayo,shule hiyo ilikuwa na upungufu wa madawati  118 ambapo madawati yaliokuwepo yalikuwa ni 103 na kwamba hivi sasa  kutokana na msaada wa madawati hayo,hakuna tena upungufu wa madawati katika shule hiyo.

Diwani wa Kata ya Muhukuru Manufred Mzuya anasema kabla ya msaada wa madawati 150 kutoka Benki ya NMB,shule hiyo ilikuwa inakabiliwa na upungufu wa madawati hali ambayo ilikuwa inaathiri taaluma kwa wanafunzi katika shule hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI RUVUMA

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma Awapongeza Wastaafu 86 wa Kada ya Ualimu Mkoani Ruvuma

    May 08, 2025
  • Kamati ya Siasa Wilaya Yaridhishwa na Hatua za Miradi ya Maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

YALIYOJIRI MAKABIDHIANO YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa