• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NMB yaipiga jeki shule ya Msingi Ndelenyuma mabati 175

Tarehe ya kuwekwa: October 29th, 2019

BENKI ya NMB imetoa msaada wa mabati 175 ya geji 28 yenye thamani ya shilingi milioni tano katika shule ya Msingi Ndelenyuma iliyopo katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza kabla ya kukabidhi bati hizo katika hafla ambayo imefanyika katika shule ya Msingi Ndelenyuma,  Meneja wa NMB Kanda ya Kusini Janeth Shango amesema kwa miaka kadhaa sasa NMB imekuwa mstari wa mbele kuchangia miradi ya mbalimbali ya  maendeleo.

“Mpaka ninavyoongea leo, kwa mwaka huu 2019 pekee,tayari tumetoa misaada yenye thamani ya shilingi milioni 710,tumejikita zaidi kwenye miradi ya elimu na afya’’,amesema Shango.

Hata hivyo amesema katika miradi ya elimu NMB imejikita katika  madawati na vifaa vya kuezekea na katika sekta ya afya wamejikita kwenye  vitanda na magodoro yake .

Kulingana na Meneja huyo wa NMB Kanda ya Kusini,kwa mwaka 2019 Benki hiyo imetenga bajeti ya  zaidi ya shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya jamii katika sekta ya elimu na afya.

Kwa upande wake Mgeni rasmi katika Hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema ametoa rai  kwa watanzania kuitumia  Benki ya NMB kwa kuwa imezifikia wilaya zote nchini kwa asilimia 100 na kwamba inatoa huduma za kibenki kwa mitandao ambazo zinapatikana kwa wananchi wengi zaidi mijini na vijijini.

“Mimi kama Mkuu wa Wilaya kwa niaba ya wananchi wa Madaba na Wilaya ya Songea nawashukuru NMB kwa msaada wenu ambao mmekuwa mnautoa kwetu mara kwa mara’’,amesema Mgema.

Hata hivyo amesema NMB imekuwa msaada mkubwa katika wilaya ya Songea ambapo mwaka 2018 walitoa msaada  wa vitanda na magodoro katika kituo cha Afya Madaba na kwamba NMB pia ilitoa msaada wa meza,viti na madawati kwa shule za msingi na sekondari zilizopo katika Wilaya ya Songea.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Madaba Vastus Mfikwa amesema msaada huo umekuja wakati muafaka kwa sababu kijiji hicho ni kipya na usajiri wake hauzidi miezi miwili hivyo msaada huo unatatua changamoto ya vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya Msingi Ndelenyuma.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Ndelenyuma  Beneth Mwamjembe ameishukuru Benki ya NMB kwa msaada huo ambao amesema unakwenda kutatua changamoto ya mradi wa vyumba vitatu vya madarasa unaoendelea katika shule hiyo.

Amesema mradi vya vyumba hivyo ambao ulianzishwa mwaka 2018 bado haujakamilika na kwamba shule hiyo yenye wanafunzi 68, ilianzishwa mwaka 2014.

Imeandikwa na  Albano Midelo

Afisa Habari Serikalini

Oktoba 28,2019

 

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa