• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NMB yazipiga jeki shule mbili za sekondari Songea

Tarehe ya kuwekwa: January 16th, 2020

BENKI ya NMB imetoa msaada wa madawati bora 60  na viti vyake 60  kwa ajili ya shule ya sekondari ya Magingo iliyopo katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Akitoa taarifa ya Benki hiyo kwenye hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliyofanyika katika shule ya msingi Magingo Madaba,Meneja wa NMB Kanda ya Kusini  Haji Msingwa amesema NMB pia imechangia viti vya maabara 132 kwa ajili ya shule ya sekondari ya Lipupuma .

Msingwa amesema vifaa vyote hivyo vimegharimu shilingi milioni 8.5 na kwamba katika mwaka 2020,NMB imetenga bajeti ya zaidi ya bilioni moja kwa ajili ya kuchangia maendeleo ikiwemo kusaidia sekta ya afya na elimu.

“NMB itaendelea kuunga mkono juhudi za wadau wake katika kuhakikisha kuwa changamoto za jamii zinapatiwa ufumbuzi katika kujenga afya na elimu bora’’,alisisitiza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Madaba na Diwani wa Kata ya Mkongotemba Vastus Mfikwa akizingumza baada ya kupokea msaada huo ameishukuru NMB kwa kupunguza changamoto ya madawati katika shule mbili za sekondari zilizopo katika kata yake ambapo vifaa hivyo vitasaidia kuboresha elimu katika Kata hiyo.

Amesema shule ya sekondari ya Magingo ni miongoni mwa shule zilizofanya vizuri kwenye mtihani wa Taifa wa kidato cha nne ambapo Halmashauri ya Madaba imekuwa ya kwanza kati ya Halmashauri nane za Mkoa wa Ruvuma na imeshika nafasi ya 23 kitaifa kati ya Halmashauri  185 Tanzania na msaada huo utachochea zaidi katika elimu.

Afisa Elimu Kata ya Mkongotema Edwin Thadei amesema Kata hiyo ina shule mbili za sekondari  za magingo na Lipupuma ambazo zilikuwa zinakabiliwa na changamoto ya meza na viti na kwamba msaada wa  NMB umepunguza tatizo kwa asilimia 90 baada ya kutoa msaada wa meza,viti na stuli.

“Kabla ya msaada kutoka Benki ya NMB,sekondari ya Magingo na Lipupuma zilikuwa na upungufu wa meza 77,viti 87 na stuli 82’’,alisema.

Akizungumza kabla ya  makabidhiano ya vifaa hivyo ,mgeni rasmi kwenye hafla hiyo ,Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololet Mgema amesema Benki ya NMB imekuwa msaada mkubwa katika Wilaya ya Songea kwa kutatua changamoto katika sekta ya afya na elimu.

Mgema amesema  msaada uliotolewa na NMB unakwenda kuchochea ufaulu kwa wanafunzi  kwa sababu wanasoma katika madarasa yenye mazingira rafiki ya kusomea ambapo amesisiza kuwa urithi pekee kwa watoto ni elimu.

 Antony Mayemba ni mmoja wa wanafunzi katika sekondari ya Magingo ameipongeza NMB kwa msaada huo ambao amesema umepunguza changamoto ya viti na meza kwa wanafunzi.

NMB ina matawi zaidi ya 224 na wateja zaidi ya milioni tatu katika nchi nzima, ikiwa imezifikia wilaya zote kwa asilimia 100,huku ikiendelea kuboresha huduma za kibenki kwa njia ya mtandao ili kufikisha huduma za kibenki kwa wananchi wengi zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa