• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NYASA kujenga hospitali ya Wilaya inayogharimu bilioni 1.5

Tarehe ya kuwekwa: January 25th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa inatarajia kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambayo inatarajia kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni moja na nusu (1,500,000,000) itakayojengwa katika kitongoji cha Mtambo wa Lami kijiji cha Nangombo Kata ya Kilosa wilayani hapa ili kuwasogezea karibu huduma ya matibabu wananchi wa Wilaya ya Nyasa.

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Dkt Oscar Mbyuzi wakati akiongea na wananchi wa Kitongoji cha Mtambo wa Lami, kijiji cha Nangombo Kata ya Kilosa, wakati akiwapa taarifa ya kukamilika kwa Taratibu kwa kuanza ujenzi wa majengo saba ya Hospitali ya Wilaya ya Wilaya ya Nyasa.

Dkt Mbyuzi alifafanua kuwa Wilaya ya Nyasa inakusudia kuanza ujenzi wa hospitali ya Wilaya itakayojengwa katika kitongoji cha Mtambo wa lami katika kijiji cha Nangombo Kata ya kilosa ujenzi ambao unatarajia kuanza kesho kwa kusogeza miundombinu ya maji na kuanza ujenzi huo mara moja kwa kuwa tayari serikali imeshaleta fedha kiasi cha tsh (1,500,000,0000/=) bilioni moja na nusu kwa ajili ya ujezi wa hospitali hiyo.

Aliyataja majengo yanayaoanza kujenga kuwa ni Jengo la utawala,Jengo la wagonjwa wan je(OPD),Jengo la stoo ya Dawa,Jengo la Maabara,jengo la vipimo vya mionzi(x-ray)Jengo la kufulia nguo(Laundry) na jengo la wazazi.

Aliongeza kuwa Taratibu zote za kuanza ujenzi zimekamilika ikiwa ni pamoja na kutangaza matangazo ya kutafuta fundi wa kujenga majengo ya hospitali hiyo na kuwashirikisha wananchi wa wilaya hii ili washiriki kikamilifu katika zoezi hili la ujenzi wa hospitali kwa kuwa kuna mafundi kujenga na wafanyakazi mbalimbali watahitajika na kipaumbele kitatolewa kwa wakazi wa wilaya ya Nyasa ili waweze kufanya kazi na kuongeza kipato kupitia kazi mbalimbali watakazokuwa wanazifanya katika eneo hilo la ujenzi.

Hapo awali Wilaya ya Nyasa ilikuwa haina Hospitali ya Wilaya hivyo ilikuwa inawalazimu wananchi kutembea umbali wa kilometa 66 kwenda  Hospitali ya Wilaya ya Mbinga kupata huduma za afya kwa kuwa hapa Nyasa kulikuwa na kituo cha afya cha Mbamba-bay ambacho kilikuwa hakiwezi kutoa huduma za afya zinazopatikana katika Hospitali za Wilaya.

Mbunge wa Jimbo la Nyasa ambaye pia na Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha za ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Nyasa kwa kuwa amewajali sana wananchi wa Nyasa na hivyo kuwaondolea kero ya kupata matibabu mbali na nyasa hivyo aliahidi kusimamia vizuri ujenzi huu na kuhakikisha unakamilika kwa wakati ili kuwaondolea kero wananchi wanaotembea umbali wa kilometa 66 kufuata huduma hizo kati hospitali ya wilaya ya Mbinga na kuongeza msongamano wa hali ya juu katika Hospitali hiyo.

“Namshukuru sana mheshimiwa Rais kwa kunipa fedha za ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Nyasa ambayo itawasaidia wananchi wangu kwa kuwa walikuwa wakiteseka wakisafiri takribani kilometa 66 kufuata matibabu katika wilaya ya mbinga kama unavojua mtu akiumwa atalazimika kutafuta nauli na kutembea umbali mrefu kufuata matibabu katika hospitali ya Wilaya hasa akina mama wajawazito ambao mara baada ya kukamilika hospitali ya Wilaya ya Nyasa itawaondolea usumbufu huo”.

Mhandisi Manyanya bado aliomwomba Rais kuona uwezekano wa kumwongezea  fedha za ujenzi wa kituo kimoja cha afya katika kata ya Kingerikiti tarafa ya Mpepo ambapo kuna ongezeko kubwa la watu na wanauhitaji mkubwa wa kituo hicho cha afya. wakati akiwa katika ziara ya siku kumi katika Tarafa ya Mpepo Wilayani hapa hivi karibuni wananchi wa kata ya Kingerikiti kupitia kwa  Diwani wao wa kata ya kingerikiti mh. Alto Komba  walimwomba Mbunge Manyanya kuwajengea kituo cha afya kwa kuwa nao wanapata mbali huduma za afya.

IMETOLEWA NA

NETHO C.SICHALI

AFISA HABARI

WILAYA YA NYASA

0743615706

TAREHE 24/01/2019

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa