• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

ONGEZEKO la bei ya mazao ya nafaka SODECO laleta neema Songea

Tarehe ya kuwekwa: August 7th, 2019

WAFANYABIASHARA wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamepata neema kutokana na ongezeko la bei ya mazao katika soko la la mazao ya wakulima (SODECO) lililopo mjini Songea.

Katibu Mkuu wa umoja wa wanunuzi mazao vijijini Mkoani Ruvuma Thadey Mwakaguo akizungumza katika mahojiano ofisini kwake mjini Songea,amesema bei ya Mahindi kwa mwaka huu inaridhisha ukilinganisha na msimu uliopita.

Bei ya mahindi katika msimu wa mwaka 2018/2019 imepanda kutoka shilingi 400 kwa kilo hadi kufikia shilingi 600 hali ambayo imeleta neema kwa wananchi wa wilayani Songea na Mkoa wa Ruvuma kwa ujmla.

Kwa mujibu wa Mwakaguo,zao la  mahindi  kwa mwaka 2019 limeuzwa kwa asilimia 50 mwanzoni mwa msimu ukilinganisha na mwaka jana 2018 mauzo yalikuwa  asilimia 50 kwa msimu mzima.

Mwakaguo amezitaja changamoto wanazopata katika soko lao  kuwa ni  kukosekana kwa maghala ya kuhifadhia mazao yao,wakulima kutozingatia ubora na viwango vya mazao wanayozalisha na kusababisha  kushuka kwa soko hilo hali inayosababisha  mazao kununuliwa kwa bei ya  chini.

“Kutokana na kushuka kwa bei ya mahindi mwaka jana kulisababisha baadhi ya  wakulima kususia na kukata tamaa kuzalisha zao hilo kwa wingi.”Amesema Mwakaguo

Hata Hivyo,Mjasiliamali Joseph Komba amesema kuwa suala la bei ya mazao kuwa nzuri lina manufaa kwa upande wao na kuomba Serikali kupunguza ushuru na kuwapa mikopo itakayowasaidia kuboresha shughuli zao.

“Tunalipa ushuru mara mbili kutoka kijijini hadi sokoni ukiachana na ushuru mdogomdogo unaotozwa ndani ya soko.”amesema Komba

Naye, Mkulima Benae Lwosu ameshukuru kupanda kwa bei ya mahindi na ametoa wito kwa Serikali kuboresha bei ya mazao mengine kama vile soya na kuwepo kwa soko huria litakalomruhusu mkulima kuuza  soya mwenyewe.

Soko la SODECO linauza na kununua mazao mbalimbali kama vile Soya,mbaazi,mahindi na maharage.

Imeandaliwa na

Bacilius kumburu

Wa kitengo cha TEHAMA Manispaa ya Songea

Agosti 6, 2019.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Chupa 14,789 za Damu Kukusanywa Mkoani Ruvuma

    June 04, 2025
  • Mazishi ya Muasisi wa TANU Alhaji Mustapha Songambele

    June 03, 2025
  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • Tazama zote

Video

katibu Mkuu CCM Taifa Aongoza Maziko ya Alhaji Songambele
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa