• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Songea Municipal Council
Songea Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu ya Msingi
      • Mazingira na Usafi
      • Maji
      • Afya
      • Elimu ya Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi
      • Fedha na Biashara
      • Arthi na Mipangomiji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Legal Services
      • Mawasiliano, Habari na Teknolojia
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma zetu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi isiyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAIS ATOA DAWA YA KUTOKOMEZA MBU SONGEA

Tarehe ya kuwekwa: September 29th, 2017

Rais Magufuli atoa dawa kutokomeza mbu Songea

SERIKALI imeongeza chachu katika mapambano dhidi ya malaria baada ya kununua lita laki moja za dawa za kuua mbu na kusambazwa kote nchini ili kukabiliana na malaria.
Viuadudu vya kutokomeza mbu wa malaria vinatengenezwa katika kiwanda cha kuzalisha Viuadudu kilichopo Mjini Kibaha mkoani Pwani.

Halmashauri 14 nchini ikiwemo ya Manispaa ya Songea zina viwango vikubwa vya maambukizi ya ugonjwa wa malaria,tayari Manispaa ya Songea imepokea dawa hiyo na hivi sasa yanafanyika maandalizi ya kuanza kupulizia makazi ya wananchi ili kutokomeza ugonjwa huo.

Afisa Afya na mazingira wa Manispaa ya Songea Dk.Vitalis Mkomela amesema manispaa ya Songea imepokea lita 1000 za dawa hiyo ambazo zimenunuliwa na Rais Dk.John Magufuli ambapo kiasi hicho cha dawa kinatosha kupulizia kipindi hiki cha kiangazi katika mitaa 95 ya manispaa hiyo.

Amesema kabla ya kuanza kazi ya kupulizia hivi sasa yanaandaliwa mafunzo na miongozo kwa wafanyakazi wa kujitolea 95,wenyeviti wa mitaa 95 na maafisa afya ambao watapewa kwanza elimu ili waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.

“Idara itanunua pampu 98 zitakazotumika katika zoezi hilo,pia inahitajika usafiri ili  wafanyakazi waweze kuanza kazi mapema kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa tano kabla ya jua la utosi’’,anasema.

Hata hivyo amesema mazalia ya mbu yakipingua,mbu wa malaria pia watapungua na hatimaye ugonjwa wa malaria kupungua na kutokomezwa katika Manispaa ya Songea.

Ili kuhakikisha zoezi hilo linatoa matokeo makubwa Dk.Mkomela amesisitiza kuwa kila dimbwi lenye mazalia litapuliziwa mara nne kwa mwezi sawa na kupulizia mfululizo kila baada ya siku saba na kwamba  watapulizia mazalio ya mbu yaliyofunikwa na mazalio ya mbu yaliowazi.

Amesisitiza kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu ambapo katika kipindi cha masika manispaa itanunua dawa za kupulizia mazalio yote ambayo yatakuwepo katika kipindi hicho ili kuhakikisha kuwa mazalia ya mbu yanatokomezwa katika manipaa hiyo.

Jumla ya watu 133 katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea wamefariki dunia mwaka 2015 baada ya kuugua ugonjwa wa malaria.Watanzania 60,000 wanakufa kila mwaka kutokana na ugonjwa wa malaria ambapo kila siku nchini watu 291 wanapoteza maisha kutokana na malaria.

Matangazo

  • TANGAZO LA LESENI ZA BIASHARA January 22, 2025
  • TANGAZO la usafi wa mazingira Jumamosi ya mwisho wa mwezi Septemba 2024 February 27, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • TAKUKURU Mkoa wa Ruvuma Yafanikiwa Kurejesha Mil. 9.2, na Kudhibiti Mianya ya Rushwa.

    May 30, 2025
  • TAKUKURU Ruvuma Yawezesha kupatikana fedha za makusanyo Songea Dc

    May 30, 2025
  • ALAT Ruvuma na Baraza la Madiwani la Chalinze Watembelea Manispaa ya Iringa Kujifunza Ukusanyaji wa Mapato.

    May 29, 2025
  • ISMAIL ALI MKIMBIZA MWENGE KITAIFA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ALAT RUVUMA ZIARANI IRINGA TC
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Ruvuma Region Website
  • Songea diistrict websites
  • Madaba District Council Website
  • Tunduru District Website
  • Namtumbo District Website
  • Nyasa District Website
  • Mbinga Town Council Website
  • Mbinga District Council Website
  • Songea Municipal face book

Tovuti Mashuhuri

  • Wizara ya Fedha
  • TAMISEMI
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • National Bureau of Statistics
  • Baraza la Mitihani Tanzania

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    SONGEA MUNICIPAL COUNCIL

    Anuani ya Posta: P O BOX 14, SONGEA

    Simu ya Mezani: 025 2602970

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@songeamc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Songea. Haki zote zimehifadhiwa